DC DENDEGO KUFUNGUA PAZIA LA LIGI YA UVCCM CUP MABAWA

November 01, 2013


Na Oscar Assenga,Tanga.
MKUU wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Ligi ya Umoja wa Vijana kata ya Mabawa (UVCCM)itakayoanza kutimua vumbi Jumapili wiki hii kwenye viwanja wa soka Mikanjuni Sekondari.

Akizungumza leo,Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mabawa, Ramadhani Hanaph alisema maandalizi ya kuelekea mashindano hayo yanaendelea vizuri na kinachosubiriwa ni kuanza kwake.

Hanaph alisema mashindano hayo yatashirikisha timu kumi na tatu ambazo zitagawanywa katika makundi mawili ambayo itachezwa kwa mfumo wa ligi.

Alisema mashindano hayo yatafunguliwa Jumapili kuanza majira ya saa tisa mchana ambapo zitaanza shamrashamra kwa timu zote kumi na tatu kujipanga kwenye mstari ili kusubiri kukaguliwa na mgeni rasmi.

Mwenyekiti huyo alisema lengo la mashindano hayo ni kuinua vipaji katika kata hiyo na kuhamasisha vijana kupenga michezo na kujiepusha kutumia madawa ya kulevya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »