ROSTAM AZIZ NDIYE BABA WA MATAJIRI WOTE TANZANIA, MENGI WA PILI AFRIKA NZIMA KATIKA WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI

November 16, 2013

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam 

TANZANIA imeongoza katika orodha ya tatu ya matajiri wapya wakubwa Afrika iliyotolewa na jarida la Forbes, mfanyabishara Rostam Aziz aliyeacha siasa kwa shinikizo la chama chake, CCM ili kubaki kwenye biashara pekee akitajwa kuwa tajiri zaidi nchini.

Rostam aliyejiuzulu Ubunge wa Igunga mwaka 2011, jarida la Forbes limesema ana utajiri wa thamani ya dola za Kimarekani Bilioni 1. 
Mtanzania tajiri zaidi; Rostam Aziz ana zaidi ya dola Bilioni 1

Rasilimali zake kubwa ni pamoja asilimia 35 ya hisa katika kampuni ya Vodacom Tanzania, kampuni kubwa ya simu za mkononi Tanzania, ikiwa na wateja zaidi ya milioni 9.5; kampuni ya madini ya Caspian Mining, pamoja na biashara anazofanya kwa kushirikiana na  na bilionea wa Hong Kong, Li Ka-shing. Azizi pia amewekeza Dubai na Oman.

Mtanzania mwingine, Reginald Mengi ni tajiri mkubwa wa pili Afrika katika uwekezaji kwenye sekta ya Habari, baada ya Koos Bekker wa Afrika Kusini. Binafsi, Mengi anamiliki kampuni ya IPP yenye magazeti 11, Televisheni tatu na vituo 10 vya Redio. 

Rasilimali nyingine za Mengi ni migodi ya dhahabu, kampuni kadha za madini na kampuni ya soda ya Coca-Cola. Ana utajiri wa jumla ya dola za Kimarekani Milioni 550 kwa mujibu wa tathmini za FORBES.

Mtu mpya katika orodha ya matajiri 50 wa Forbes 50 ni Mualgeria, Issad Rebrab, ambaye ameingia na tajiri wa thamani ya dola Milioni 3.2. Rebrab ni muanzilishi wa Cevital, kampuni ya familia inayotengeneza sukari, mafuta ya kupikia na jibini. Cevital pia inamiliki viwanda vya uzalishaji bidhaa za kusambaza.

Bilionea wa Kenya na Afrika Mashariki, Vimal Shah ameingia kwenye orodha hiyo na utajiri wake wa dola Bilioni 1.6. Shah, baba yake na kaka yake kwa pamoja wanamiliki kampuni ya mafuta ya kupikia Bidco. 

Pato la mwaka la kampuni hiyo ni dola Mlioni 500. Bidco pia inatengeneza unga wa chakula na sabuni za manukato katika nchi 14 Afrika. Pia ni muwekezaji wa Tatu City, kampuni mpya yenye thamani ya dola Bilioni 3  ya Satellite itakayokuwa na maskani yake, Nairobi.

Mmorocco, Aziz Akhannouch ana utajiri wa dola Bilioni 1.4 kutokana na kumiliki kwake kampuni ya Akwa Group, iliyoanzishwa na baba yake ambayo kwa sasa inamiliki kampuni za Afriquia Gas na Maghreb Oxygene pamoja na vyombo vya habari, uwekezaji wa ardhi na hoteli. Akhannouch kwa sasa ni Waziri wa Kilimo na Uvuvi wa Morocco. Mkewe, Salwa Idrissi, anamiliki majengo ya kifahari.

Aspen Pharmacare, walioshiriki kuanzisha Gus Attridge ya Afrika Kusini wameingia kwenye orodha hiyo kwa utajiri wao wa dola Milioni 525.

Mtanzania, Mohammed ‘Mo’ Dewji anaingia katika orodha hiyo kwa utajiri wake wenye thamani ya dola milioni 500. Ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya METL, iliyoasisiwa na baba yake, Gulam Dewji. 

Baada ya kumaliza masomo ya biashara katika chuo Kikuu cha Georgetown, Marekani alirejea nyumbani kuendeleza biashara za baba yake na pia kwa sasa ni mwanasiasa, Mbunge wa jimbo la Singida Mjini.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »