NA BONIFACE WAMBURA,DAR ES SALAAM.
Baraza
la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA)
limefungua maombi ya vitambulisho (Accreditation) kwa ajili ya waandishi
wa habari wanaotarajia kuripoti mashindano ya Kombe la Chalenji.
Mashindano
ya Kombe la Chalenji yatafanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 hadi
Desemba 12 mwaka huu. Kwa waandishi wa habari wanaotaka kuripoti
mashindano hayo wanatakiwa kutuma maombi yao kabla ya Oktoba 31 mwaka
huu.
Mbali
ya majina, katika maombi hayo mwandishi wa habari ni lazima aoneshe
chombo anachofanyia kazi na kuambatanisha na picha moja ya pasipoti.
EmoticonEmoticon