HALMASHAURI YA SIHA MKOANI KILIMANJARO INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA WATUMISHI 379

October 04, 2013
NA OMARY MLEKWA.
WAJUMBE wa Baraza la Madiwani Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro limeiomba serikali  kutoa kibali kwa halmashauri nchini  kuajiri watumishi ili  kukabiliana na uhaba wa watumishi katika halmashauri zote kwa madhumuni ya kuleta maendeleo zaidi.
 
Ombili hilo limetolewa  katika  kikao cha baraza maalumu la Madiwani wilayani Siha cha kupokea taarifa ya hoja za mkaguzi wa hesabu za serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2011/2012  ambapo wameiomba serikali kuwapatia kibali cha kuajiri watumishi  ili kuboresha huduma kwa wananchi
 
Halmashauri hiyo  inakabiliwa  na upungufu wa watumishi 379 wa idara mbalimbali hali inayochangia zaidi   kuzorotesha maendeleo ya halmashauri hiyo.
 
Wakizungumza katika baraza hilo wajumbe hao walisea baadhi ya hoja zilizotolewa na mkaguzi wa serikali zimechangia na upungufu wa watumishi idara mbalimbali kutokana na watumishi kuzidiwa na kazi wanazofanya isiyoendana  kasi ya ongezeko la wananchi pamoja na miradi inayotekelezwa katika wilaya ya hiyo
 
Akichangia hoja hiyo, Makamu Mwenyekiti  wa Halmashauri hiyo Dancan Urasa alisema kutokana na upungufu walionao katika kitengo cha ukaguzi wa ndani kumesababisha kuwepo kwa hoja ambazo zingeweza kutatuliwa na wakaguzi hao kwa kushirikiana na wataalamu wengine
 
Alisema kitengo hicho kwa sasa kinawatumishi wawili tu hali ambayo inakuwa shida kukaguzi shughulizote zinazotekelezwa  ndani Wilaya na kuiomba wizara husika kuwapatia kibali cha kuajiri angalau mtumishi mwingine mmoja ili kuimarisha kitengo hicho
 
Urassa alisema ikiwa halmashauri zitapewa mamlaka ya kuajiri watumishi zitaweza kukabiliana na changamoto hiyo kwa kuwa watumishi watakaoajiriwa watachukuliwa wakiwa wanatambua mazingira wanayokwenda kufanyia kazi kwenye halmashauri husika .
 
Awali akiwakilisha hoja za mkaguzi  hesabu za  serikali  kwa niaba ya mkaguzi mkazi ofisi ya Taifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali mkoani Kilimanjaro,Fredi Mapunda alisema wilaya hiyo katika ukaguzi ilipata hoja 38  ambapo hoja nane zilifungwa kutokana na kudhirishwa  na majibu yaliyotolewa na wataalamu
 
Mapunda alisema halmashauri hiyo ihakikishe kuwa inafuatilia maoni ya mkaguzi ambapo mkaguzi aliwashauri kukumbushia ofisi ya Rais  menejment na utumishi wa Umma na Wizara ya fedha kuruhusu kupata kibali cha kuajiri
 
Akijibu hoja hizi mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Siha, Rashidi Kitambulio alisema walishaandika barua kwa katibu mkuu Menejment ya utumishi wa umma na kupatiwa watumishi wa 70 wa idara ya elimu  na 19 wa idara ya afya  na halmashauri imeshatuma barua ya ajira mbala kwa ajili ya kukabiliana na changamoto hiyo
 
Alibainisha kuwa athari zinazotokana na upungufu huu wa watumishi ni utoaji wa huduma usioridhisha, pamoja na watumishi kukosa ari ya kufanya kazi kwa kuwa mtumishi mmoja kwa wastani anafanya kazi ya watu wawili hadi watatu jambo ambalo huchangia ucheleweshaji wa shughuli nyingi za kimaendeleo ndani ya halmashauri hii.
 
Hata hivyo wajumbe hao walishauri serikali  baadhi ya kada ya ajira zake zifanywe na halmashauri  ili kuweza kuwapata watumishi hao ikiwemo ajira za watendaji wa kata na kijiji  badala ya ajira hizo kutolewa na Menejmenti ya Utumishi wa Umma pekee

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »