HALL MECHI YETU NA COASTAL UNION KESHO ITAKUWA NGUMU.

October 04, 2013
NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
KOCHA Mkuu wa timu ya Azam FC "Wanarambaramba"Stewart Hall amesema mechi yao ya Ligi kuu Vodacom Tanzania bara dhidi yao na Coastal Union itakayochezwa Jumamosi katika uwanja wa Mkwakwani itakuwa ngumu kutokana na Coastal Union kuwa na sapoti kubwa ya mashabiki hasa inapokuwa ikicheza nyumbani.

Hall alitoa kauli hiyo wakati wa mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini hapa na kuelezea maandalizi kwaupande wao yanaendelea vema licha ya kuwa na wachezaji wenye majeraha madogo madogo ambao huenda wakacheza mechi hiyo.

Aliongeza kuwa licha ya kuwa na sapoti lakini ni timu nzuri hivyo
watahakikisha wanafanya kazi ya zaida ili kuweza kupata ushindi kwenye mchezo huo ambao unatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa.

   "Tunajua Coastal Union inasapoti kubwa sana ya mashabiki hasa
wanapokuwa wakicheza nyumbani hivyo sisi tunahitaji kujiandaa vya kutosha ili kuweza kupata ushindi kwa kucheza kwa umakini
mkubwa"Alisema Hall.

Hall alisema mchezaji kwenye majeraha ambaye huenda akaukosa mchezo huo ni mlinda mlango wao Aishi Manula ambaye pia amewasili mkoani hapa akiwa na wenzake.

Azam Fc imetua juzi jijini Tanga ikiwa na wachezaji wake wote na
imekuwa ikifanya mazoezi katika uwanja wa Mkwakwani ambapo mashabiki nawapenzi wa soka mkoani hapa wamekuwa wakijitokeza kushuhudia mazoezi hayo.

Wakati Azam Fc ikifanya mazoezi Mkwakwani wapinzani wao Coastal Union wao wanaendelea na mazoezi yao katika uwanja wa soka Disuza ikiwana wachezaji wake wote kamili kuweza kuwakabili wanaramaramba hao.

Katika mechi hiyo viingilio vinatarajiwa kuwa sh.7000 na 5000 mzunguko ili kuweza kuiwapa fursa wadau wa soka mkoani hapa kuweza kupata nafasi ya kuitazama mechi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »