TUPO IMARA KUPAMBANA NA AZAM FC-MORROCO

October 04, 2013
NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
KOCHA MKUU wa Timu ya Coastal Union ya Tanga,Hemed Morroco amesema kikosi cha timu kipo tayari kuwavaa wapinzani wao Azam Fc katika mchezo wa Ligi kuu Tanzania bara ambao utachezwa kesho kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini hapa.

Morroco alitoa kauli hiyo leo wakati wa mazoezi ya asubuhi ambapo timu hiyo inajifua katika uwanja wa soka Disuza ikiwa na wachezaji wake wote lengo likiwa ni kuhakikisha wanapata ushindi kwenye mpambano huo utakaochezwa saa kumi kamili za jioni Jumamosi hii.

Akizungumza hali za wachezaji,Morroco alisema wapo imara na wanaendelea kufanya maandalizi yao ya mwisho kabla ya kuwakabili wanarambaramba hao ambapo alisema wamepania kuibuka na ubingwa kwenye mchezo huo.

Morroco alisema wachezaji wake wote wanaendelea vizuri na mazoezi na wapo imara kuweza kuwakabili wapinzani wao hao isipokuwa mchezaji wao Abdi Banda ambaye anasumbuliwa na majeraha madogo madogo lakini akaongeza kuwa upo uwezekano mkubwa wa kucheza mechi hiyo.

Morroco aliongeza kuwa watahakikisha kuwa wanacheza kufa na kupona ili kuweza kupata pointi tatu muhimu kwenye mchezo huo ambao unatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa.


Kwa upande wake,Msimamizi wa kituo cha Tanga,Khalid Abdallah alitaja viingilio kwenye mechi hiyo kuwa ni 7000 na 5000 mzunguko ili kuweza kuwapa fursa wadau wa soka kuhudhuria mchezo huo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »