COASTAL UNION:HATUJAMFUKUZA MOROCO MKATABA WAKE UMEKWISHA.

October 18, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
MJUMBE wa Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Coastal Union ya Tanga, Albert Clement Peter “Mkubwa wa Kazi amekanusha vikali taarifa zilizosambazwa na baadhi vyombo vya habari kuwa wamemfukuza kocha wao mkuu Hemed Morroco.

Akizungumza na Blog hii, Peter alisema wao hawajamfukuza kocha huyo kama ilivyoripotiwa bali mkataba wake wa kuendelea kuinoa timu hiyo umekwisha hivyo wataangalia hatima yake kama watamuongezea au la.

Alisema hivi sasa kocha huyo yupo mjini Bukoba akiwa na kikosi cha timu hiyo wakijiandaa na mechi yao dhidi ya Kagera Sugar ambayo itachezwa Jumamosi hii kwenye dimba la soka la Kaitaba.

 “Mimi nashangaa sana kusikia baadhi ya vyombo vikiripoti tumemfukuza Morroco hizo habari wamezitoa wapi jamani acheni uzushi Morroco bado ni kocha wetu na yupo na timu bukoba “Alisema Peter.

Mjumbe huyo alisema uongozi wa klabu hiyo umeshapitisha jina la msemaji wao na hivyo wanatarajia kumtangaza muda wowote ambaye atachukua nafasi ya Edo Kumwembe.

Alisema mkataba wa kocha huyo uliisha tokea mwanzoni mwa mwezi huu ambapo bado uongozi haujakaa naye na kuzungumza kuhusiana na mkataba mpya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »