30 WAITWA ZANZIBAR HERROES

October 22, 2013
Na Masanja Mabula .Zanzibar .
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Zanzibar Salim Nassor Bausi ametangaza majina ya wachezaji 30 ambao wataunda timu ya Zanzibar Herroes kitachakashiriki michuano ya challange .

Katika kikosi hicho Majina yaNahodha wa timu hiyo na msaidizi wake  Nadri Haroub Kanavaro na Agrey Morris yakiwa  hayamo huku pia kukiwa na mchezaji mmoja pekee kutoka timu za Pemba zinazoshiriki ligi kuu ya Zanzibar .

Makipa walioitwa kuunda timu hiyo ni Mwadin Ali kutoka Azam ,Abdalla Rashid Ruvu Shooting pamoja na Ali  Suleiman  kutoka timu ya Miembeni .

kwa upande wa walinzi ni Mohammed Azan kutoka Polisi  , Waziri Salum Azam , Shafi Hassan Malindi , Mohammed Faki Zimamoto , Salum Haji Miembeni , Said Yussuf Mtende Rangers , Mohamed Othaman kutoka Jamhuri ya Pemba , Mussa Said Chwaka Stars pamoja na Nassor Massoud Cholo Simba .

Viungo ambao wameitwa na kocha Bausi ni Abduhalim Humud ,Simba ,  Sabri Ali, JKT Oljoro , Adeyoum Saleh , Simba ,Is-haka Othaman JKU , Ali Kani JKT Oljoro , Hamad Mshamata Chuoni , Salum Hamad Miembeni , Awadh Juma , Mtibwa Sugar , na Masoud Ali Mtibwa Sugar .

Washambuliaji ambao wamepewa jukumu la kuhakikisha kwamba n yvu za timu pinzani zinapata hujuma kila wakati ni Seif Abdalla ,Azam Suleiman Kassim Serembe Coastal Union ,Khamis Mcha Azam , Amour Omar Miembeni , na Amir Hamad JKT Oljoro .

Wengine ni Jaku Joma Mafunzo , Faki Nahoda Kimbuga , Hassan Seif  Mtibwa Sugar pamoja na Juma Ali kutoka klabu ya New Geeration .

Kwa mujibu wa kocha bausi ni kwamba timu hiyo itaingia kambini Novemba 15 huku pia akiitaka ZAF kuandaa michezo mingi ya kirafiki kabla ya kuielekea Kenye kwa ajili ya michuano hiyo .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »