Shirikisho la waislamu lafuturisha Tanga

July 27, 2013
Na Burhan Yakub,Tanga.
Shirikisho la Taasisi za Kiislamu Mkoa wa Tanga(SHITA),limetimiza miaka mitano tangu kuanzishwa kwake   likiwa limefanikiwa kuondoa tofuati za kimitizamo zilizokuwa zikiwagawa waisamu miaka ya nyuma.

Kuondolewa kwa tofauti hizo kumewezesha waislamu wa Mkoa wa Tanga kujenga mshikamano uliodumisha amani  na hivyo kuwashangaza wengi waliokuwa wamezoea kushuhudia mitafaruku ya mara kwa mara.

Mwenyekiti wa Shirikisho hilo,Omari Guledi alitoa taarifa hiyo jana jioni alipokuwa akizungumza na waislamu waliohudhuria futari iliyoandaliwa na Shita Jijini hapa.

“Shita ilipokuwa ikianzishwa miaka mitano iliyopita wengi walidhani haitafanikiwa chochote lakini hivi sasa imejenga mshikamano miongoni mwa taasisi zilizokuwa zikipingana na kusababisha waislamu kuwa kitu kimoja”alisikika akisema Guledi.

Katibu wa shirikisho hilo,Ahmed Mustaffa alisema baada ya kufanikiwa kuziunganisha taasisi hizo,hatua inayofuata sasa kwa Shita ni kuanza kuzijengea uwezo wa kiuchumi ili ziweze kujiendesha zenyewe badala ya kutegemea misaada .

Katika hafla hiyo viongozi wa taasisi mbalimbali za kiislamu waliipongeza Shita kwa kuwaunganisha waislamu kuwa kitu kimoja licha ya kuwa hijitokeza tofauti ndogondogo lakini hukaa pamoja na kuzitatua.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »