IMEWEKWA saa 01:44.
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
TIMU
ya soka Kwamichi Fc juzi ilifanikiwa kuchukua pointi tatu muhimu kwenye
mechi yao na Mirada Fc baada ya kuibamiza mabao 3-0,ikiwa ni muendelezo
wa michuano ya kombe la Sheshe Cup inayoendelea kutimua vumbi uwanja wa
Chuda relini jijini Tanga.
Katika
mchezo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa licha ya Kwamichi Fc kuonekana
kuutawala mchezo huo kwa kiasi kikubwa na kupata bao lao la kwanza
dakika ya 6 kupitia Omari Daiyo bao ambalo lilidumu mpaka timu zote
zinakwenda mapumziko.
Mpaka
timu zote zinakwenda mapumziko,Kwamichi walikuwa wakiongoza ambapo
kipindi cha pili kilianza kwa kasi kubwa kutokana na timu zote kufanya
mabadiliko.
Wakionekana
kuukamia mchezo huo,Kwamichi waliweza kujipanga na kuweka safu imara
ambayo iliweza kuwadhibiti wachezaji wa Mirada Fc hali iliyopelekea
kuwachezesha nusu ya uwanja.
Kutokana
na hali hiyo,Kwamichi waliweza kufanya shambulio la nguvu langoni mwa
wapinzani wao na kuweza kufanikiwa kuandika bao la pili kwenye dakika ya
75 ambalo lilifungwa na Omari Bakata baada ya kutumia uzembe wa mlinda
mlango wa timu ya Mirada na kuweka wavuni mpira huo.
Katika dakika ya 85 Yasini Baba Yero aliweza kuwainua kwenye
vitini mashabiki wa timu ya Kwamichi mara baada ya kuifungia bao la tatu ambalo liliweza kuihitimisha karamu ya mabao.
Mratibu
wa Ligi hiyo,Mbwana Sir Ride aliliambia gazeti hili lengo la kuanzishwa
mashindano hayo ni kutaka kuibua vipaji vya wachezaji wachanga na
kuinua kiwango cha soka.
EmoticonEmoticon