BARAZA LA WAKULIMA LALAMIKIA BAJETI

June 20, 2013

Na Oscar Assenga,Tanga.
Baraza la Wakulima Tanzania limeeleza kusikitishwa kwake nas namna ambavyo Bajetion ya serikali iliyosomwa hivi karibuni ilivyoendnelea kuwapuuza wakulima pamoja na Baraza hilo kupeleka mapendnekezo yao kwa serikali.

Mwenyekiti wa Baraza hilo, Salum Shamte akitoa maoni ya Baraza katika mahojiano  na vyombo vya Habari alisema kuwa Bajeti ya mwaka huu, pamoja kutangaza neema kwa kuanza kwa Benki ya Wakulima ambayo ilikuwa kilio kikubwa cha wakulima, bado haijagusa masuala nyeti kwa wakulima kama vile suala la muda mrefu la kupunguza mzigo wa kodi kwa nia ya kuwawezesha wakulima kuongeza tija, uwekezaji, mapato na hatimaye kuondo umaskini.

“Kodi hizo maranykingine zinaongezwa kineyemela na kimya kimya bila serikali kufanya majadiliano na wadau,” alilalamika Mwenyekiti huyo.

Alisema kuwa kama Tanzania inataka kuleta mapinduzi ya kijani katika kilimo lazima iwe makini katika suala la kuondoa kero ya kodi nyingi kwa wakulima na wazalishaji wengine.

Shamte alitoa mfano wa ushuru wa mazao unatozwa na halamshauri za serikali za mitaa ambao alisema wakuilma wamalazimika kulipa ushuru wa asilimia 5 ambao ni mara 17 zaidi ya wenye viwanda ambao hulipa ushuru wa huduma wa aslimia 0.3. “Hii haieleweki, haielezeki na haikubaliki,” alisema Mwenyekiti huyo.

Alibainisha kuwa Baraza limefanya utafiti kuta kujua kama mapato hayo yanayopkusanya na Halmshauri yanafika katika hazina za halmashauri hizo. “NI asilimia 67 tu ya makusanyo hayo ya ushuru ambayo yanafika halmashauri na fedha nyingine zinayeyuka kastika mifuk ya wajanja,’ alieleza.

Alisema serikali lazima isikie kilio cha wakulima na kuchukua hatua kuhus kodi hiyo kwa mujibui w a maepndekezo ili kuleta tija wa wakulima.

Shamte pia alieleza kuhusu kupanda kwa kiasi kikubwa kwa kodi ya aardhi mwaka jana mwezi Agosti ambapo kodi hiyo imepnda kwa asilimia 500 kutoka Sh. 200 kwa hekta hadi Sh. 1,000 ka hekta kwa walioko maeneo ya vijijini na Sh. 10,000 kwa hekta kwa mashamba ambayo yako maeneo yaliyoko chini ya mamlaka za miji kwa wale ambao wana hati.

Alisema kuwa kodi hiyo hailipiki kwa sababu kama wakulima watalipa kodi hiyo na nyingine zinazowakabili basi watafunga shughuli zao. Alitoa mfano wa Ranchi ya Ruvu ambayo alisema hivi sasa inatakiwa kulipa Sh. milioni 107  kwa mwaka hata kabla hawajaanza kuuza ndama.

Akizungumzia mkonge, Shamte ambaye pia ni Mkrugenzai Mtendaji wa Kampuni ya Mkonge wa Katani Limited ya Tanga, alisema kuwa sekta ya mkonge italazimika kulipa jumla ya Sh.Bilioni 1.18 kwa mwaka kama kodi ya ardhi kutoka Sh. Milioni 87 iliyokuwa ikilipa awali.

Pia alizungumzia ongezeko la kutisha la kodi ya OSHA ambayo imepandishwa kutoka Sh. 5,000 kwa mfanyakaazi hadi Sh. 40,000 kwa mfanyakazi kwa mwaka jambo ambalo kwa mfano katika sekta ya mkonge itaifanya ilazimike kulipa jumla ya Sh. Bilioni 14 kwa mwaka kwa ajili ya kodi hiyo tu.

Alitaja pia kodi ya huduma za zimamoto ambayo imepanda kutoka Sh. 200,000 kwa mwaka hadi kufikia Sh. milioni 2 kwa mwaka . alisema kuwa kdo hiyo kwa mashamba mengi haina maana sana kwa sababu yako mabli sana na huduma hiyo.

Shamte pia alilalamikia ongezeko la mamfuta ya diseli ambayo amesema kuwa ndio roho kwa kwa sababu hahwatumii mafuta hayo kwa usairishaji tu bali katika utayaruishaji wa mashamba, jambao ambalo litaongeza gharama za uendeshaji wa mazao na kuua faida kwa wakulima pamoja na kushindwa katika  ushindani na bidhaa kama hizo katika soko la kimataifa.

Alisema kuwa katika nchi nyingine kilimo kinapewa upendeleo fulani kwa kuondoa kodi kanma hizo ili kuongoeza tija.

Mwenyekiti huyo, wakati huo aliitaka serikali kuhakikisha kuwa inapopunguza kodi jambo hilo linatekelzw ipasavyo. Alitoa mfano kuwa nmawka jana serikali ilipunguza kodi kwa vipuri lakini hadi  hivi kodi hiyo inaendele kutozwa.

MWISHO

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »