WATANZANIA MILIONI 37 KUPIGA KURA TAREHE 29 OKTOBA, 2025

July 26, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.



******************
Na. Mwandishi Wetu
Tarehe 29 Oktoba, 2025 ndio siku ya Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Madiwani kwa Tanzania Bara. Jumla ya Wapiga Kura 37,655,559 wamejiandikisha.
 
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele leo tarehe 26 Julai, 2025 kwenye hafla ya uzinduzi wa ratiba ya uchaguzi iliyofanyika kwenye makao makuu ya Tume, Njedengwa jijini Dodoma.
 
“Tarehe 09 Agosti, 2025 hadi tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais. Tarehe 14 Agosti, 2025 hadi tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani na tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais, uteuzi wa wagombea ubunge na uteuzi wa wagombea udiwani,” amesema Jaji Mwambegele na kuongeza…..
 
“Tarehe 28 Agosti, 2025 hadi tarehe 28 Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za uchaguzi kwa Tanzania Bara. Tarehe 28 Agosti, 2025 hadi 27 Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za Uchaguzi kwa Tanzania Zanzibar ili kupisha kura ya mapema na Tarehe 29 Oktoba, 2025 siku ya Jumatano itakuwa ndiyo Siku ya Kupiga Kura”.
 
Akazingumza kuhusu idadi ya wapiga kura waliojiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi huo, Jaji Mwambegele amesema jumla ya wapiga kura 37,655,559 wamejiandikisha na kuongeza kuwa idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 26.55 kutoka idadi ya wapiga kura 29,754,699 waliokuwa kwenye daftari, mwaka 2020.
 
Ameongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar, Wapiga Kura 725,876 wapo katika Daftari la Wapiga Kura la Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na wapiga kura 278,751 wameandikishwa na INEC kwa kuwa hawakuwa na sifa za kuandikishwa na ZEC.
 
“Katika idadi ya wapiga kura 37,655,559 waliopo katika daftari, wapiga kura 36,650,932 wapo Tanzania Bara na wapiga kura 1,004,627 wapo Tanzania Zanzibar,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Ameongeza kuwa kati ya wapiga kura hao, 18,943,455 ni wanawake sawa na asilimia 50.31 na wapiga kura 18,712,104 ni wanaume sawa na asilimia 49.69 na wapiga kura 49,174 ni watu wenye ulemavu.
 
Amesema jumla ya vituo 99,911 vitatumika kupigia kura ambapo vituo 97,349 vitatumika kwa ajili ya kupigia kura kwa Tanzania Bara na vituo 2,562 vitatumika kwa ajili ya kupigia kura kwa Tanzania Zanzibar.
 
“Idadi hii ya vituo 99,911 ni sawa na ongezeko la asilimia 22.49 ya vituo vya kupigia kura 81,567 vilivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020,” amesema.
 
Jaji Mwambegele ametoa wito kwa wadau wote ikiwa ni pamoja na wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maelekezo yatakayotolewa na Tume.

WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUFANYA VIKAO NA VYAMA VYA SIASA

July 26, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 23, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga kuanzia Julai 21 hadi 23 mwaka huu.  (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 23, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga kuanzia Julai 21 hadi 23 mwaka huu.  (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Mafunzo Ndg. Faustine Lagwen, akizungumza jambo. 

Washiriki wakifuatilia ufungaji wa mafunzo hayo. 

Washiriki kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu wakifuatilia ufungaji wa mafunzo hayo.
Na. Mwandishi wetu.
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewaelekeza watendaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kufanya vikao na viongozi wa vyama vya siasa kujadili masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa uteuzi wa wagombea unafanyika kwa mujibu wa sheria.

Maelekezo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele wakati akifunga mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi mkoani Shinyanga leo Julai 23, 2025.

Mtatakiwa kuyatafsiri mafunzo haya kwenye usimamizi wenu wa shughuli za kila siku za masuala ya uchaguzi kwa kuanza na vikao na vyama vya siasa, utoaji wa fomu za uteuzi na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge na kuhakikisha utoaji wa fomu za uteuzi na uteuzi wenyewe ngazi ya udiwani ufanyike kwa mujibu wa sheria,” amesema.

Amewaelekeza kuitisha na kuratibu kamati za upangaji wa ratiba za kampeni na kuitisha kamati za maadili iwapo kuna changamoto zitajitokeza wakati wa kampeni.

Jaji Mwambegele amewakumbusha watedaji hao kuhusu wajibu wao wa kutoa mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya vituo na kuratibu na kusimamia vizuri na kwa weledi uchaguzi ngazi ya vituo.

Mafunzo mtakayowapa yatawawezesha kuratibu na kusimamia uchaguzi ngazi ya kata vizuri na kwa weledi. Hivyo, jukumu lenu ni kutoa mafunzo sahihi, kwa kuonesha kwa vitendo yote wanavyotakiwa kuyafanya wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata,” amesema.

Akifunga mafunzo kama hayo Kisiwani Pemba, Zanzibar, Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk amewakumbusha watendaji hao wajibu wao wa kubandika mabango, orodha ya majina ya wapiga kura na matangazo au taarifa zinazopaswa kuwafikia wapiga kura kwa kuwa ni takwa la kisheria na kanuni zinazosimamia uchaguzi.

“Ni wajibu wenu kuhakikisha mabango, matangazo, orodha ya majina ya wapiga kura na taarifa yoyote inayotakiwa kubandikwa kulingana na kalenda ya utekelezaji wa majukumu ya uchaguzi inabandikwa ili kuepusha malalamiko ya ukiukwaji wa masharti ya sheria na kanuni za uchaguzi,” amesema.

Amewasisitiza watendaji hao kutoa taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari ili kuwajulisha wananchi na wadau mambo mbalimbali ya uchaguzi.

“Hakikisheni mnajiandaa kabla ya kukutana na vyombo vya habari. Pima taarifa yako unayotaka kuitoa kabla hujaitoa ili kuepuka kuleta taharuki badala ya utulivu katika eneo lako na Taifa kwa ujumla,” amesema.

Mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tatu kwenye mikoa mbalimbali nchini na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo.

Tume iliyagawa mafunzo hayo kwenye awamu mbili ambapo awamu hii ya pili ilihusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi, Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.

Awamu ya kwanza ilifanyika tarehe 15 hadi 17 na ilihusisha watendaji kutoka mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Geita, Kagera, Mtwara, Lindi, Tabora, Kigoma, Tanga, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa na Njombe.
Mwisho.

MRADI WA SEQUIP KUMKOMBOA MTOTO WA KIKE DAR ES SALAAM NA RUVUMA

July 26, 2025 Add Comment
Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia Mradi wa kuboresha elimu ya sekondari-SEQUIP imekamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika shule mpya za Sekondari za wasichana Dar es salaam na Ruvuma.

BI.SAKINA MWINYIMKUU: JENGENI UTAMADUNI WA UTENDAJI UNAOTEGEMEA MATOKEO

July 25, 2025 Add Comment


*Dodoma, Julai 25, 2025*  

Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bi. Sakina Mwinyimkuu, amewataka watumishi wa umma kutumia maarifa waliyopata katika mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini ili kuongeza uwajibikaji na ufanisi katika kazi zao.

Akifunga rasmi mafunzo hayo ya siku tano yaliyofanyika jijini Dodoma, Bi. Sakina amesisitiza umuhimu wa kujenga utamaduni wa kazi bora unaozingatia matokeo (results-based performance), kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

> “Mafunzo haya si kwa manufaa yenu binafsi pekee, bali yatumike kama nyenzo ya kuleta mabadiliko chanya katika taasisi zenu, sambamba na kuendeleza maadili ya uwajibikaji,” amesema Bi. Sakina.

Ametoa rai kwa washiriki kuwa mabalozi wa kueneza uelewa huo kwa wengine katika maeneo yao ya kazi, ili kuimarisha utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia viwango vya kitaifa vya ufuatiliaji na tathmini ya maendeleo.





BENKI YA CRDB YATOA MADAWATI 111 NA KUCHANGIA UJENZI WA UZIO SHULE YA SEKONDARI PROF. ADOLF MKENDA, ROMBO

July 25, 2025 Add Comment

 


Mkuu wa Wilaya Rombo, Raymond Mwangwala (watatu kulia) akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru (wapili kushoto) kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa uzio wa Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Sambambama na hilo, pia Benki ya CRDB imekabidhi madawati 111 yenye thamani ya shilingi milioni 10, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia uwekezaji unaolenga sekta muhimu za afya, elimu na mazingira ambayo asilimia 1 ya faida baada ya kodi hutengwa kila mwaka kwa ajili ya kusaidia miradi ya kijamii yenye tija. Mchango huu unalenga kuhakikisha ushiriki wa Benki ya CRDB katika kukuza elimu na kuboresha mazingira ya kusomea yaliyo salama. Wengine pichani ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat (kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rombo, Emmanuel Sindiyo (kulia) pamoja na Afisa Tawala wa Rombo, Isack Martin.

Mkuu wa Wilaya Rombo, Raymond Mwangwala (kulia) akipokea moja ya madawati kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru kwa ajili ya Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat.
Mkuu wa Wilaya Rombo, Raymond Mwangwala akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Burudani pamoja na wanafunzi