Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE AWASILISHA SALAMU ZA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA RAIS WA UGANDA MHE YOWERI KAGUTA MUSEVENI JIJINI KAMPALA LEO

April 08, 2025 Add Comment

 

Pembenzoni mwa Mkutano wa Uongozi wa Afrika wa nane jijini Kampala Uganda leo, Mheshimiwa  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwa kama mjumbe maalum, amewasilisha ujumbe maalum kwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kutoka kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. 


Rais Museveni alimshukuru Dkt Kikwete kwa kumtembelea na kumuomba amfikishie salamu zake kwa Mheshimiwa Rais Samia na watu wa Tanzania.



MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI UTOAJI WA TUZO ZA UANDISHI BUNIFU

April 07, 2025 Add Comment

 NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV


MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha Utoaji wa Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu ambayo itafanyika Aprili 13,2025 kwenye ukumbi wa The Super Dome Masaki Jijini Dar es Salaam..

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 7, 2025 Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, Prof. Penina Mlama amesema vigezo vilivyotakiwa kutumika katika kushiriki kushindania Tuzo hiyo vilitangazwa kna pia mwitikio mwaka huu ni kama ilivyokuwa miaka miwili ya nyuma, umekuwa mzuri.

Amesema Tuzo hiyo kwa Mwaka huu wa 2024 /25 inahusisha nyanja nne za ushairi, riwaya, hadithi za watoto na tamthiliya.

"Utaratibu wa zawadi kwa washindi utabaki kama ilivyokuwa miaka iliyopita yaani, Mshindi wa kwanza Shilingi milioni 10, Muswada wake utachapishwa na serikali na kusambazwa shuleni na maktaba za taifa, Ngao na Cheti. Mshindi wa Pili atapata Shilingi milioni 7 na Cheti, pia Mshindi wa tatu nae atapata Shilingi milioni 5 na Cheti". Ameeleza Prof. Mlama.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa serikali inataka kuhamasisha utamaduni wa kusoma vitabu nchini ndio maana wanaelea kuhamasisha watu waweze kutenga muda wa kujisomea vitabu.

"Watanzania wengi hawana utaratibu wa kujisomea vitabu, hivyo tunaamini kwa kutumia waandishi wetu nchini wataweza kuandika vitabu na kuhamasisha watu kusoma vitabu". Amesema Prof. Mkenda.

Amesema kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa mwandishi mzuri aliweza kuandika vitabu mbalimbali  na namna amechangia kukuza lugha ya kiswahili hivyo kumuenzi kwake wameamua siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake kuwepo kwa utoaji wa tuzo hizo.










WAKULIMA WA MWANI, WAVUVI MKINGA WALISHUKURU SHIRIKA LA TAWSEI KUWAPATIA ELIMU

April 07, 2025 Add Comment




Na Oscar Assenga, MKINGA



WAKULIMA wa Kilimo cha Mwani na Wavuvi kata ya Manza na Mayomboni wilayani Mkinga Mkoani Tanga wamelishukuru Shirika la Tanzania Women For Self Initiatives (TAWSEI) kwa kuwapatia elimu juu ya umuhimu wa Amani  wakati wa utekelezaji wa shughuli zao kutokana na mgogoro baina yao

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mkutano wa kata ya Mayomboni wilayani kupitia mradi wa  Amani ni Tunu ambao ulitokana na mradi mkubwa wa "Kujenga Amani Pamoja "kupitia warsha zilizofanyika kwa kushirikiana na Shirika la 4 H Tanzania,We Word na Taswei kupitia ufadhili wa Umoja wa Mataifa ya Ulaya.

Ambapo kulibainika mgogoro mkubwa baina ya wakulima wa Mwani na Wavuvi kutokana na shughuli zao kufanyika katika moja la bahari ya Hindi.

 ambapo walisema elimu ambayo wameipata itawawezesha kutekeleza vema majukumu yao na hivyo kuweza kujiongezea pato na kukuza uchumi wao.



Akizungumza katika mkutano huo Baraza Seif ambaye ni Mkulima wa Mwani kutoka Kijiji cha Ndumbani aliwashukuru kwa kupatiwa elimu hiyo wakulima wa mwani na wavuvi ambayo itafungua ukurasa mpya katika shughuli zao

Alisema athari kubwa wanayokumbana nayo ni wavuvi wa nyavu aina ya kokoro waliopo kwenye maeneo ya Kata ya Moa na wavuvi wachache wanaotumia nyavu hizo kwenye kata ya Mayomboni na kutumia utupa ambao unaathiri Mwani wao.



“Hii ndio changamoto kubwa kwetu sisi wakulima hivyo Tunawaomba waache kwani kilimo cha Mwani kina faida kubwa kwenye maeneo sana ndani ya kata na nchi kilimo cha mwani ni zao endelevu mpaka kupelekwa nje “Alisema


Alisema kwamba jambo ambalo wanaliomba ni kuwepo kwa elimu endelevu kuhusu namna ya kuacha kuharibu zao za mwani kutokana na umuhimu wake katika kuwaingizia kipato cha mtu mmoja moja na jamii kwa ujumla.



“Tunaomba Shirika hili liweze kusimamia na kuturekebisha eneo hilo katika kata hizo mbili kutokana na baadhi yao kulima Mwani na wengine kuvua kwenye mashamba ya yao jambo ambalo linaleta uvunjifu wa amani wakati wa utekelezaji wa shughuli zao na kuathiri mkulima wa mwani kutokana na kwamba wanakwenda kuvua usiku.


Maeneo yanayolimwa mwani samaki wengi wanapwenda kwenda kuvua hapo hivyo wanaomba wavuvu waendele kupewa elimu kama wanahusika na mambo hayo waache maana kilimo cha mwani wanakitegemea kuendesha maisha yao na familia zao.



Naye kwa upande wake Mvuvi Salim Jumaa alisema kwamba kero yao watu wa mwani wanasema wavuvi wanaharibu mwani sio kweli kwa sababu hao watu wa mwani maeneo ambayo wavuvi wanayafanyia kazi wameyazuia na kuweka vigongo vyao ..

Hata hivyo Mkulima wa Mwani Kata ya Mayomboni Faida Bakari alisema wavuvi wanaposema wanawakosea maana wao ndio wana haribu kilimo cha Mwani kutokana wanapofika kwenye maeneo ya mashamba ya mwani wanang’oa vigongo na kuziachia kamba zinatembea.



“Sisi tunapoteza nguvu zetu unasema kuna kamba kumi unakuta zimeng’olewa na wanaweka utupa kuvua.hivyo tunaomba itungwe sheria ya kudhibiti vitendo vya namna hiyo katika maeneo yetu”Alisema


Kwa upande wake Mkazi wa Mayomboni Rehema Ally alisema athari kubwa ni wavuvi wa kukoro na wavuvi wanaotumia vyombo vikubwa na hivyo kuharibu mwani wao na mabadiliko ya tabia ya nchi yamewaathiri sana hivyo wanaiomba serikali wanapotoa malalamiko yao wapatiwe ufumbuzi hasa wale wanaovua uvuvi haramu.



Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahandakini Jasiri Nassoro Mbaraka alisema kwamba wanakuwa na makosa wakulima kama wanajua watu wanaoharibu mashamba yao ili pawe pazuri wanatakiwa wawaripoti kwenye vyombo vya kisheria.


“Lakini pia waweke hadharani kwanini mmetoka kule mnakuja kuvua huku kokoro ilipigwa marufuku isivue wanaowazungumza wavuvi wanavua kandondao ya kisiwa vya Kirui na kuna mashamba ya mwani na maeneo hayo yamewekewa zuio wasivue nadhani tunakuwa na makosa wakulima maeneo hayo yamewekewa zuio yasivuliwe na wanawaficha ili waweze kupata amani wakamatwa wafikishwe kwenye vyombo vya sheria”Alisema



Alisema kwani kuvua uvuvi haramu na kuharibu mashamba wakiendelea kuwaficha wavuvi wataharibu amani na haitapatikana mpaka wapelekewe kwenye vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua ili kukomesha vitendo vya namna hiyo kwenye mashamba ya mwani .



“Tukiendelea kuwaficha mgogoro huu hauwezi kupata ufumbuzi ili tutatue migogoro sheria zitumike wakulima wa mwani mnaona watu wanaharibu mwani mnaacha kuwasema sio sawa kwa maana palipowekewa zuio popote haparuhusiwi kufanya shughuli za uvuvi”Alisema



Akizungumza mmoja wa viongozi wa Shirika la Tawsei alisema lengo la mkutano huo ni kuana namna ya kupata ufumbuzi wa amani iliyopo nchini hivyo wanalishukuru Shirika la 4h Tanzania na wafadhili We World kushiriki pamoja kwenye mkutano huo.

Aidha pia walipendekeza kuwepo na ufumbuzi wa kutatua migogoro baina ya wakulima wa mwani na wavuvi wa samaki ili kudumisha na kuendeleza amani ya nchi y.  

Mradi huo unatekelezwa wilaya ya Mkinga katika kata mbili za Mayomboni na Manza ambao utakuwa chachu ya kutoa elimu itakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na tija zaidi.



Mwisho.

WAISHUKURU TAASISI YA UMOJA WA WASAIDIZI WA SHERIA UWASHEM KUWAWEZESHA KUTATUA MIGOGORO BAINA YA WAVUVI NA WAKULIMA WA MWANI

April 07, 2025 Add Comment

 


WANANCHI wanaofanya shughuli za  Uvuvi na Wakulima wa Zao la Mwani wanaoishi katika kijiji cha Mwaboza wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga wameishukuru taasisi ya Umoja wa wasaidizi wa Sheria 'UWASHEM' kwa kuwawezesha kutatua mgogoro baina yao kutokana na matumizi ya rasilimali bahari ambapo kupitia elimu waliyoipata imewawezesha kuwaunganisha.


Awali wakizungumza katika mdahalo wa pamoja  ulioandaliwa na taasisi hiyo kwa lengo la kutambua changamoto zilizopo baina yao Kila mmoja ameonekana kumshutumu mwingine kuwa chanzo cha mgogoro kwa kile walichoeleza kuwa wamekuwa wakigombania maeneo hali iliyopelekea kukosa maelewano na hatimaye kuwaingiza kwenye mgogoro.

Wakizungumza baadhi yao wamesema kuwa pamoja na elimu waliyoipata kupitia shirika la UWASHEM' ni vyema Serikali ikatenga maeneo maalum ili kuwasaidia wananchi hao kufanya shughuli zao bila bughuza  na hatimaye kuendelea kujipatia kipato Chao cha Kila siku

Mratibu wa miradi kutoka shirika la UWASHEM' Swalehe Sokolo amesema kuwa  kupitia mradi huo wanaoutekeleza imesaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto baina ya Wavuvi na Wakulima wa Zao la Mwani ambapo pia wameweza kuwaunganisha na viongozi wa Serikali.

Kwa upande wake mratibu wa mradi wa KUJENGA AMANI PAMOJA kutoka shirika la shirika la We World  Zacharia Msabila amesema wanafanya kazi na  taasisi zilizopo karibu na jamii ambapo kupitia ufadhili wanaoutoa itasaidia kufikia malengo waliyoyatarajia.

Diwani wa kata ya Moa Staruki Njama amekiri uwepo wa migogoro ya muda mrefu biana ya Wakulima wa Zao la Mwani na Wavuvi katika kijiji cha Mwaboza ambapo shirika la UWASHEM' limekuja kuleta suluhisho kupitia elimu waliyoitoa ambapo amewapongeza kwa jitihada walizozifanya huku akisisitiza  wananchi kuendelea kufuatia na kutekeleza Sheria zilizowekwa.

Shirika la umoja wa usaidizi wa Sheria Mkinga "UWASHEM'' linatekeleza mradi wa KUJENGA AMANI  PAMOJA katika wilaya hiyo kwa kushirikiana na shirika la 4H Tanzania  ukifadhiliwa na shirika la We World kwa lengo la kuleta amani baina ya wananchi kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani.

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA RAIS DKT SAMIA SULUHU KUANZA RASMI MKOA WA TANGA APRILI 8 MWAKA HUU

April 04, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA

KAMPENI ya Msaada wa kisheria ya Rais Dkt Samia Suluhu “Mama Samia Legal Aid Campaign” inatarajiwa kuanza kutoa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi wanaokabiliwa na migogoro mbalimbali ikiwemo ya ardhi kuanzia Aprili 8 mwaka huu mkoani Tanga huku wananchi wakihimizwa kujitokeza kwa wingi.

Msaada huo wa kisheria utaongozwa na Jopo la wataalamu zaidi ya 40 kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za Kisheria kupitia kliniki ya utatuzi wa msaada wa sheria ya Rais Dkt Samia Suluhu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian alisema uwepo wa kampeni hiyo katika Mkoa Tanga utasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua migogoro iliyopo ambayo mingine imedumu kwa muda mrefu .


Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wananachi kuchangamkia fursa hiyo na kwamba mkoa huo utatoa ratiba maalumu ya wapi wananchi watatakiwa kwenda kwajili ya kukutana na jopo hilo la wataalamu ili kupata ufumbuzi wa migogoro yao huduma ambayo itatolewa bila gharama yeyote

Aidha alisema kampeni hiyo itazinduliwa katika viwanja vya Tangamano na itajumuisha Halmashauri zote za Mkoa wa Tanga pamoja na kwensa kwenye ngazi za chini hadi ngazi ya kata,vijiji na mitaa.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga alisema lengo la kampeni hiyo ni kuongeza uelewa wa masuala mbalimbali ya kisheria ili jamii iweze kutambua hasa katika haki za wanawake, watoto, wazee, watu wenye ulemavu na makundi yote kwa ujumla wake.

Alisema jambo la pili kwenye kampeni hiyo ni kuimarisha huduma ya ushauri wa kisheria kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia, wengi wakiwa watoto, wakina mama na wakina baba.

Mkuu huyo wa mkoa alisema jambo la tatu ni kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu elimu ya sheria kwa uma, masuala ya haki na wajibu pamoja na misingi mizima ya utawala bora, hiku suala la nne likiwa kutoa elimu ya usimamizi wa mirathi na masuala mazima ya urithi wa ardhi ,haki ya kumiliki mali.

"Jambo la tano ni utatuzi wa migogoro kwa viongozi wa serikali za mitaa, watendai wa kata , vijiji, wajumbe wa mabaraza ya ardhi kwa kushirikiana na wazee maalumu , machifu, viongozi wa dini na serikali, nipongeze sana timu hii nimeambiwa kwambackambi hii arusha imeweza kutatua mgogoro uliodumu kwa takribani miaka 27,"Alisema Mkuu huyo wa Mkoa.



Akizungumza wakati wa mkutano huu na waandishi wa habari Mratibu wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoa Tanga ambaye ni Afisa Uchunguzi Mkuu kutoka Wizara ya Katiba ya Sheria Laurent Burilo alisema katika maeneo mengi waliyokwisha kuyafikia changamoto kubwa zilizojitokeza ni migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ni kilio kwenye maeneo mengi.

Aliongeza kwamba jambo jingine ni masula ya ndoa na matunzo ya watoto ikiwemo mirathi ambalo nalo limeweza kujitokeza kwenye maeneo mengi.

Akitolea mfano Burilo alisema Mikoa 23 ambayo wameifikia wamekumbana na migogoro mingi kwa mfano Mikoa 22 ambayo wameifikia wamefanikiwa kuwafikia wananchi zaidi ya milioni 2 huku wakikumbana na migogoro zaidi ya elfu ishirini kati ya migogoro hiyo migogoro zaidi ya 4000 imetatuliwa na kuisha kabisa ambapo wamekumbana na migogoro mingine ambayo imedumu kwa zaidi ya miaka kumi hadi 20