Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

MARA WARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI YA REA

March 29, 2025 Add Comment


📌 Wamshukuru Rais Samia kwa kupunguza gharama za umeme


📌 Elimu kuhusu matumizi bora ya nishati yatolewa


📌 Watakiwa kuchangamkia fursa ya kuunganisha umeme


Wananchi mkoani Mara wamesisitiza kuridhishwa na utekelezaji miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), inayotekelezwa nchini kwa lengo la kuwapatia umeme wa gharama nafuu, na wameipongeza Serikali kwa kuwafikishia miradi hiyo muhimu yenye faida kwa uchumi wa Taifa.

Pongezi hizo zimetolewa na wananchi kwa Wataalam wa REA waliofika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kutumia fursa ya miradi ya REA inayotekelezwa katika Kata ya Kwangwa wilaya ya Musoma mkoani Mara. 


Aidha, wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia fedha REA kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya umeme mkoani humo.


Awali Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka REA, Abdulrazack Mkomij ametoa elimu kwa umma kuhusu gharama za kuunganisha umeme, matumizi bora ya nishati, kuhamasisha kuunganisha umeme, tahadhari za umeme na elimu kuhusu utunzaji wa miundombinu ya umeme. 

Naye, Mhandisi wa Miradi ya REA mkoa wa Mara, Omary Gwillah, amesema kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya umeme mkoani humo ili wananchi wafanye shughuli zao kwa tija. 

Kwa upande wake, Mtendaji wa Kata ya Kwangwa, Bwiso Kinanda, ameishukuru Serikali kwa kupunguza gharama za uvutaji umeme. Amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ya uvutaji wa umeme. 

Vile vile, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kwangwa B, Maxmilian Kunju akizungumza kwa niaba ya wananchi ameiomba REA kuendelea kufikisha umeme kwenye maeneo mengine mkoani humo ili wananchi wa Musoma wapate nishati ya umeme.


TANESCO YAANZA KAMPENI YA KUTOA ELIMU YA USALAMA KWENYE MATUMIZI YA UMEME MIKOA YA KANDA YA ZIWA

March 29, 2025 Add Comment


📌Kampeni inalenga kuelimisha watoto kuzingatia usalama kwanza watumiapo umeme. 


📌Itasaidia Kupunguza athari na ajali zitokanazo na majanga ya umeme kwenye Mikoa hiyo.

Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO) Machi 27 limeanza kampeni maalumu ya kuelimisha juu ya kuzingatia usalama kwanza kwenye matumizi ya Umeme kwa Makundi ya watoto katika shule mbalimbali za msingi zilizopo kwenye mikoa ya Mara, Kagera, Mwanza, Geita na Simiyu.

Kampeni hiyo inayoitwa " Zingatia Usalama Kwanza Utumiapo Umeme" inalenga kuwafikia wanafunzi wa shule za msingi na kuwapa elimu inayowawezesha kugundua vihatarishi vinavyoweza kusababisha ajali zinazotokana na majanga ya umeme na kuepuka  athari zitokanazo na majanga hayo.

Akizungumza katika moja ya Shule zilizotembelewa Kaimu Meneja Masoko kutoka TANESCO Bwana Sylvester Matiku amesema elimu hiyo ni muhimu kuwalinda watoto na majanga ya umeme kutokana na kuwa kati ya makundi yanayopata athari zaidi na ajali za umeme.

''Shirika limeona lianze kampeni hii hasa kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa kutokana na hivi karibuni kuwa na matukio ya ajali zitokanazo na umeme zinazoathiri zaidi watoto na hivyo tukaona tuje kuwaelimisha ili kusaidia kupunguza na kuondoa madhara ya ajali zitokanazo na umeme''.

Wanafunzi hao wamepatiwa elimu kuhusu Matumizi Sahihi ya Umeme ili kuokoa gharama pamoja na kuitambulisha namba mpya ya ya huduma kwa wateja bila malipo ya Mchongo 180.

Katika kampeni hiyo Wanafunzi katika  shule mbalimbali wamepata fursa ya kuhoji maswali kuhusu umeme na athari za umeme na jinsi ya kumsaidia muathirika wa ajali za umeme.

Wanafunzi hao wameahidi kufikisha elimu waliyoipata kuhusu Umeme na Usalama katika Kampeni ya hiyo kwa familia zao, ndugu, jamaa na marafiki na wameomba elimu hiyo pia ifikishwe kwa Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum.

Kampeni hii muhimu inaendelea kwenye mikoa yote Kwenye Kanda ya Ziwa.



KAMPUNI YA SUNKING YAUNGA MKONO AGENDA YA RAIS SAMIA

March 28, 2025 Add Comment

 

Kampuni ya sola ya SunKing imeendelea kusogeza karibu zaidi huduma kwa wananchi baada ya kufungua duka jipya katika eneo la stendi ya Kona ya Kayenze jirani na Kisesa, Wilaya ya Magu mkoani Mwanza.

Akizungumza Ijumaa Machi 28, 2028 wakati wa hafla ya ufunguzi wa duka hilo, Msimamizi wa Biashara wa kampuni hiyo, Juma Mohamed amesema hadi sasa jumla ya maduka 65 yamezinduliwa kote nchini na mkakati ni kuendelea kufungua maduka zaidi ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

"Kazi yetu ni kubuni, kutengeneza na kusambaza mitambo inayotumia nishati ya jua (sola) yenye uhakika wa mwanga ang'avu na salama kwa matumizi ya wananchi. Hili litakuwa duka la nne Mwanza ambapo tayari tumefungua Buhongwa, Buzuruga, Buswelu" alisema Mohamed.

Mohamed amebainisha kuwa kampuni hiyo ina mitambo ya gharama nafuu inayotolewa kwa mkopo kuanzia shilingi 350 kwa siku huku ikiwa na mitambo yenye uwezo wa kuwasha vifaa mbalimbali ikiwemo taa, TV na friji.

Ameongeza kuwa kampuni ya SunKing inaunga mkono jitihada za Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zinazohamasisha nishati safi ili kuondokana na matumizi ya nishati chafu hatari kwa mazingira ikiwemo mkaa, kuni na mafuta ya taa.

Akizungumza kwa niba ya Mkuu wa Wilaya ya Magu, Afisa Tarafa ya Sanjo- Perpetua Chonja amewahimiza wananchi kuepuka matumizi ya nishati chafu ikiwemo vibatari kwani moshi wake ni hatari kwa macho na mapafu na badala watumie taa za SunKing kama nishati mbadala kwa hasa umeme unapokatika.

Chonja ameipongeza kampuni ya SunKing kwa kuunga mkono jitihada za Raid Dkt. Samia ambaye amekuwa akihamasisha nishati safi ikiwemo mitungi ya gesi ambapo kwa Tarafa ya Sanjo jumla ya majiko 800 yametolewa kwa wananchi.

Kwa upande wake balozi wa SunKing, mwanamuziki Mrisho Mpoto amesema bidhaa za SunKing ni bora kwani zinatoa nishati ya kutosha hata wakati wa mawingu huku pia ikitoa fursa kwa mtu yeyote kuwa wakala wa kuuza bidhaa hizo ambapo hadi sasa ina zaidi ya mawakala elfu tatu nchini.

Nao baadhi ya wananchi akiwemo Beatrice Michael na Kipara Luhiji wamesema bidhaa za SunKing ni mkombozi hasa kwa wajasiriamali wanaofanya shughuli zao nyakati za usiku ambapo hupata mwanga ang'avu ambao pia huwasaidia wanafunzi kujisomea wakiwa nyumbani.
Na George Binagi- GB Pazzo, Mwanza
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye iliyopo Kijiji cha Isangijo Kata ya Bukandwe wilayani Magu. Wa tatu kushoto ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Wengine ni viongozi mbalimbali Kata ya Bukandwe.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye iliyopo Kijiji cha Isangijo Kata ya Bukandwe wilayani Magu. Wa tatu kushoto ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Kulia ni Balozi wa SunKing, Mrisho Mpoto.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akikata keki kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye Mwanza. Kulia ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Wengine ni viongozi wa Kata ya Bukandwe.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akimlisha keki Balozi wa SunKing, Mrisho Mpoto.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akimlisha keki mmoja wa wananchi.
Uzinduzi wa bidhaa za SunKing katika eneo la stendi ya Kona ya Kayenze Mwanza.
Wakazi wa Mwanza wakifuatilia uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo Kona ya Kayenye jirani na Kisesa.
Mmoja wa wakazi wa Mwanza akipatiwa huduma ya sola kutoka kampuni ya SunKing.

Mawakala wa SunKing wakiwa kwenye picha ya pamoja na mwanamuziki Mrisho Mpoto.
Burudani.

KAMATI YA PIC YARIDHISHWA NA THAMANI YA FEDHA KATIKA MRADI WA MAJI SAME MWANGA KOROGWE.

March 28, 2025 Add Comment

 NA WILLIUM PAUL, MWANGA.


WAJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imeridhishwa na ubora wa mradi wa maji Same Mwanga Korogwe ambao umegharimu zaidi ya Bilioni 400 na kudai kuwa thamani ya fedha inaonekana katika mradi huo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Augustine Vuma mara baada ya kutembelea mradi huo ambapo alisema kuwa, hali ya upatikanaji wa maji kwa sasa katika miji ya Mwanga na Same ni ya kuridhisha kwani wananchi wanapa maji kwa masaa 24.

“Kamati imeridhishwa na ubora wa mradi pamoja na upatikanaji wa maji kwa sasa hivyo kamati inaipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongpzwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kujenga mradi huo na zimetolewa kwa wakati” alisema Vuma.

Alisema kuwa, jukumu la sasa kwa Wizara ya maji kupitia mamlaka yake ya Mwanga Same ni kutunza mradi huo kwa kushirikiana na Wananchi ili uendelea kuwa bora na kudumu muda mrefu ili kuhakikisha kuwa wananchi hawarudi kule walipotokea kukosa maji au kupata kwa mgao.

Aidha wameiagiza mamlaka hiyokuhakikisha inatekeleza mpango wa usambazaji maji kikamilifu katika maeneo ya mamlaka ili kuwafikiwa wahitija na kutimiza adhima ya Serikali ya kuwafikia wananchi wengi huduma.

Alisema kuwa, mamlaka hiyo inatekeleza mpango wa ulinzi wa vyanzo vya maji na miundombinu yake pamoja na kuweka mpango wa muda mfupi na mrefu wa ukarabati wa miundombinu ya maji ili kuhakikisha mradi unaendeshwa kwa ufanisi na katika hali ya uendelevu ambapo jambo hilo litapelekea mradi huo kutoa tija.

“Mamlaka ya maji Same Mwanga hakikisheni mnaimarisha mkakati wenu wa ushirikiano wa kibiashara na wadau mbalimbali wakiwemo wateja wakubwa ili kuweza kuwafikia kihuduma jambo ambalo litawezesha kuongeza wigo wa kiwango cha ukusanyaji wa mapato pamoja na kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kulipia Ankara za maji kikamilifu na kwa wakati ili kuepuka changamoto za madeni ambayo imekuwa kikwazo kwa mamlaka nyingi nchini” alisema Vuma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa mamlaka ya Maji Same Mwanga (SAMWASA), Mhandisi Rashid Mwinjuma alisema kuwa, kupitia mradi huo kwa sasa wananchi wa Mwanga na Same wanapata maji ya uhakika masaa 24, ambapo hali hiyo imesaidia mapato yameongezeka kutoka milioni 40 kwa mwezi hadi kufikia milioni 70.

Mhandisi Mwinjuma alisema kuwa, hata wateja wameongezeka kutoka 4000 hadi kufikia 6000 huku akidai kuwa mwamko wa wananchi kuomba kuunganishiwa huduma ya maji umekuwa mkubwa.

“Kwa sasa tunajukumu la kuendelea kusambaza mtandao wa maji ili kuwafikia wateja wengi ili kusaidia kukusanya fedha za kuweza kuendeshea mradi huu na kwa siku tumekuwa tukipokea wastani wa watu 50 wanaotaka kuunganishiwa na huduma ya maji lakini tumeendelea kutoa elimu ili watambue umuhimu wa kulipia Ankara zao kwa wakati” alisema Mhandisi Mwinjuma.




SimBanking kugawa milioni 240, magari matano kwa wateja wake

March 27, 2025 Add Comment

Ikizindua msimu wa tano wa kampeni ya yake ya Benki ni SimBaking, Benki ya CRDB imetangaza kutenga zawadi kiasi cha shilingi milioni 240 pamoja na magari matano.
Akizindua kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul amesema kwa mwaka huu benki imejipanga kutoa magari manne aina ya Toyota IST na Toyota Harrier ‘New Model’ moja kwa wateja watakaoibuka kuwa vinara katika matumizi ya SimBanking katika kukamilisha miamala yao na huduma nyingine.

Bonaventura amesema azma ya Benki ya CRDB siku zote ni kuhakikisha inatoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja wake na jamii ya Watanzania kwa ujumla hivyo itaendelea kuwekeza kwenye ubunifu wa kidijitali ili kukidhi mahitaji yaliyopo na yatakayojitokeza.

Katika kampeni ya mwaka huu ya SimBanking amesema kutakuwa na washindi wa kila siku na kila wiki watakaopata zawadi za fedha taslimu na gari aina ya Toyota IST na mshindi wa jumla ataondoka na Toyota Harrier.

“Tumetenga zaidi ya shilingi milion 240 zitakazotolewa kwa washindi wetu na kila baada ya miezi miwili tutatoa zawadi ya gari aina ya IST wakati mshindi wa jumla tutakayemtangaza mwishoni mwa mwaka atapata gari aina ya Toyota Harrier. Magari haya yote tutakayoyatoa kwa washindi wetu ni ‘New Model’ na yamekatiwa bima kubwa. Kwa wanafunzi wa vyuo, kuna simu za kisasa aina ya Iphone 16 zitakazokuwa zinatolewa kila baada ya miezi mitatu,” amesema Bonaventura.

Kwa miaka mitano ya kuendesha kampeni ya Benki ni SimBanking, amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa ambao kwa sasa kwani kila mwezi takriban wateja milioni moja wanafanya miamala mingi kupitia programu hiyo inayowaruhusu kukamilisha malengo yao wakiwa mahali popote ndani ya saa 24.

Bonaventura amesema Benki ya CRDB inaamini katika kutoa huduma bora na za kisasa ili kuchangia maendeleo ya wateja wake na taifa hivyo kuhitaji kuwekeza katika ubunifu unaoendana na mabadiliko ya teknolojia duniani. Amesisitiza kuwa SimBanking ni kati ya huduma bora inayotambulika duniani kutokana na urahisi, usalama na uhakika wa kukamilisha miamala kidijitali.

“SimBanking ni kati ya huduma za Benki yetu ya CRDB ambazo zimeleta mapinduzi makubwa katika kuchochea ujumuishi wa huduma za fedha nchini. Kwa zaidi ya muongo mmoja sasa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2011, SimBanking imetoa fursa kwa Watanzania wengi kujiunga na mfumo rasmi wa huduma za benki.