MWALIMU ASHEHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA NA WATOTO WENYE UHITAJI ,RAIS SAMIA ATAJWA

May 17, 2025


CDE Mwalimu Nebu Malekela (katikati), wa Shule ya Msingi Magereza iliyopo Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya akikata keki wakati wa sherehe ya kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa aliyo sherehekea na watoto wenye uhitaji wanaolelewa Kituo cha malezi ya watoto hao Hospitali ya Igogwe Mei 12, 2025. Kushoto ni Mlezi wa kituo hicho, Sister Gloria Mwanjelila.

...................................

Na Dotto Mwaibale

JAMII imetakiwa kujenga tabia ya kusaidia watu wenye uhitaji hasa watoto kwani inasaidia kuwapa faraja na kujiona kama watoto wengine wanaoishi na familia zao.

Ombi hilo limetolewa na Mlezi wa Kituo cha kulea watoto wenye uhitaji katika Hospitali ya Igogwe iliyopo Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya, Sister Gloria Mwanjelila wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa Cde. Mwalimu Nebu Malekela wa Shule ya Msingi Magereza Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya iliyofanyika Mei 12, 2025.

“Hawa watoto wanahitaji faraja kama wanayopata watoto wengine katika familia zao jamii inapokuja kuwatembelea na kushiriki nao kwa mambo mbalimbali kwao inakuwa faraja kubwa na si lazima mpaka kutoa msaada wa vitu ingawa ni wa muhimu kulingana na mahitaji yao mbalimbali,” alisema Mwanjelila.

Akimzungumzia Mwalimu huyo alisema amekuwa ni mtu wa kujitoa mara kwa mara kutembelea kituo hicho na kutoa msaada kwa watoto hao na kueleza kuwa hata wakati wa kusherehekea sikukuu ya pasaka alifika katika kituo hicho na kuwaletea vitu mbalimbali akiwa ameongoza na wanajumbe Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) kutoka Kata ya Kiwira baada ya kuratibu tukio hilo.

“Hawa watoto ni wa jamii nzima na ndio tunaowategemea kuwa viongozi wa kesho sisi kama walezi wao hatuwezi kuwatoshelezea mahitaji yao yote hivyo kwa pamoja tukishirikiana tutaweza kuwapatia mahitaji yao mengine ambayo wanayakosa kutoka kwetu,” alisema mlezi huyo.

Alisema Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia Dkt. Samia Suluhu Hassan haiwezi kuvihudumia vituo vyote vyenye wahitaji hapa nchini hivyo ni vema jamii ikajenga utamaduni wa kusaidia eneo hilo ikiwa ni kuungamkono jitihada hizo za Serikali

Akizungumza wakati wa sherehe hiyo Mwalimu Nebu Malekela alisema aliona sherehe ya kumbukizi yake ya kuzaliwa afike katika kituo hicho na kusherehekea na watoto hao kwa kukata keki pamoja ambapo pia aliwapelekea zawadi.

“Lilikuwa tukio dogo lakini lenye furaha tulikata keki , tukala, kunywa, kuimba na kucheza pamoja na watoto hakika tuli ‘enjoy’sana,” alisema Mwalimu Malekela.

Ndugu zangu wanajamii Neno la Mungu linasema dunia na vyote vilivyopo ni mali ya Mungu pamoja na wewe mwenyewe na hata akiamua kuichukua mali zake atazichukua zote lakini kwa upendo mkubwa ametupa akili ya kuimiliki mali hiyo na zaidi ya yote akatupa nafasi ya kumrudishia sehemu ndogo tu ya mali zetu akituhitaji kuwasaidia wahitaji badala yake na ndio maana anatoa nafasi kwa wenye kitu kidogo kulisaidia kundi hilo kwani kutoa ni moyo na wala sio utajiri.

Mwalimu Nebu Malekela  akionesha upendo kwa kumlisha keki mmoja wa watoto wa kituo hichoMwalimu Nebu Malekela akiwa katika picha ya pamoja na watoto hao wenye uhitaji

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng