Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Kitaifa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, leo Machi 01, 2025 ameongoza kikao cha tano cha Kamati hiyo kwenye ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam.
Katika kikao hicho, Mheshimiwa Majaliwa aliimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Profesa Kitila Mkumbo, Rasimu ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 ili aipeleke kwenye Baraza la Mawaziri na Bungeni kwa ajili ya kujadiliwıa na kutungiwa sheria.
EmoticonEmoticon