WAZIRI KIJAJI AKUTANA NA KAMISHENI YA TABIANCHI YA BONDE LA CONGO

September 13, 2024

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na Waziri wa Utalii na Mazingira wa Jamhuri ya Congo ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni hiyo Mhe. Arlette Soudan – Nonault (kushto jijini Dar es Salaam. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Bi. Christina Mndeme na Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ambaye pia ni Mwakilishi wa nchi katika Mfuko wa Bluu wa Bonde la Congo Prof. Dos Santos Silayo.
Waziri wa Utalii na Mazingira wa Jamhuri ya Congo ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni hiyo Mhe. Arlette Soudan – Nonault akizungumza kwenye kikao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa kikao cha Ujumbe wake kutoka Kamisheni ya Tabianchi ya Bonde la Congo na Mfuko wa Bluu wa Bonde la Congo jijini Dar es Salaam



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Utalii na Mazingira wa Jamhuri ya Congo ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni hiyo Mhe. Arlette Soudan – Nonault (kulia) na Ujumbe wa Kamisheni hiyo jijini Dar es Salaam.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametoa wito kwa Kamisheni ya Tabianchi ya Bonde la Congo (CBCC) kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.


Amesema changamoto ya mabadiliko ya tabianchi ipo kwa maana hiyo tunatakiwa kuchukua hatua kuona dunia inakuwa salama kutokana na changamoto hiyo.


Dkt. Kijaji amesema hayo wakati wa kikao na Ujumbe kutoka Kamisheni ya Tabianchi ya Bonde la Congo na Mfuko wa Bluu wa Bonde la Congo ulioongozwa na

Waziri wa Utalii na Mazingira wa Serikali ya nchi hiyo ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni hiyo Mhe. Arlette Soudan – Nonault jijini Dar es Salaam.


Aidha, amesema katika kukabiliana na changamoto hiyo, Tanzania imekuja na biashara ya kaboni ambayo pamoja na mambo kadhaa inahusisha upandaji wa miti kwa wingi ambayo hunyonya hewa ya ukaa.


“Sisi kama taifa tumeanza kuchukua hatua kwenye biashara ya kaboni na tunatamani tuungane, tushirikiane na tunufaike kwa pamoja kubadilisha ujuzi ili tufikie malengo, tunahitaji maendele ambayo wenzetu wamepiga hatua huku wakiharibu mazingira na waathiriki wakubwa ni sisi nchi zinazoendelea,” amesema.


Mhe. Dkt. Kijaji amepongeza CBCC kwa kukubaliana namna wanavyoweza kuzisaidia nchi wanachama kupata fedha ambazo tayari zimewekwa katika Mfuko wa Bluu na benki mbalimbali wanazofanya nazo kazi kwa ajili ya kuendeleza shughuli za utalii na mabadiliko ya tabianchi.


Kwa upande mwingine amesema kama mawaziri wanaoshughulikia mazingira wana jukumu la kuhamasisha wananchi watumie niahsti safi ya kupikia badala ya kuni au mkaa ambazo zinatokana na ukataji wa miti holela.


Amesema kwa kutambua hilo tayari Tanzania imeaandaa Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia na Rais Mhe. Dkt. Samia aliamiwia na kupewa ukinara ili wananchi wanufaike lengo la kufika asilimia 80 ya kaya kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034 litimie.


Hivyo, amewapongeza wakuu wa nchi kwnye Mkutano wa COP22 kwa kuanzishwa kwa Kamisheni hiyo (CBCC) ili iangalie mabadiliko ya tabianchi na mazingira kwenye Bonde la Congo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »