JAJI MKUU AITAKA BRELA KUUNGANISHA KANZIDATA YAKE YA USAJILI WA MAKAMPUNI NA MAHAKAMA

July 06, 2024

 


John Bukuku
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ameitaka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kuiwezesha Mahakama nchini kuunganishwa kwenye Kanzidata ya Wakala ili kuweza kuhakiki taarifa za kampuni kwa uharaka pindi inapokuwa inashughulikia mashauri yahusuyo kampuni hizo

Rai hiyo ameitoa leo tarehe 5 Juni, 2024 alipotembelea banda la BRELA lilipo ndani ya jengo la Wizara ya Viwanda na Biashara katika maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara ya Dar es Salaam.

Mhe. Prof. Ibrahim Juma amesema kuwa uunganishwaji katika kanzi data itaiwezesha Mahakama kujua uhai wa kampuni na endapo imehuisha taaifa zake kwa Msajili hii itasaidia kuamua kuendelea na kesi au kusitisha endapo kampuni haijahuisha taarifa zake kwa Msajili

Aidha, Jaji Mkuu ameipongeza BRELA kwa kazi kubwa inayofanya katika kuboresha utoaji wa huduma zake kwa njia ya mtandao

BRELA inashiriki katika kutoa huduma za papo kwa hapo kwenye maonesho ya 48 ya kimataifa ya biashara ya Dar es Salaam ndani ya banda la Wizara ya Viwanda na Biashara na banda karibu na Wizara ya Fedha na Mipango

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »