SEKTA YA AFYA NEEMA TUPU MIAKA 3 YA RAIS DKT SAMIA

March 19, 2024

Na Mwandishi Wetu, Dar

Wizara ya Afya imempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluh Hassan katika kipindi cha miaka mitatu ambapo Sekta ya afya imepatiwa kiasi cha shilingi Trilion 6.722 kwa ajili ya kutekeleza vipaumbele mbalimbali ili kuimarisha huduma za afya nchini.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema wamepokea zaidi ya shilingi bilioni 20 kwenda Bohari ya Dawa MSD ili kuongeza  upatikanaji wa dawa kwenye Hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya nchini ambapo hadi kufikia Desemba 2023 zaidi ya asilimia 84 zimepelekwa kutoka asilimia 58 mwezi Desemba, 2022 na kupelekea kupungua kwa malalamiko katika hospital za umma nchini.


Ameongeza kuwa kupitia fedha hizo wizara ya afya imetekeleza kwa mafanikio makubwa majukumu yake, ikijikita zaidi kwenye maeneo ya Ujenzi wa  miundombinu ya kutolea huduma za  afya nchini, kuimarisha upatikanaji wa dawa na bidhaa nyingine za Afya.


"Ndani kipindi cha Miaka mitatau Serikali kupitia Wizara ya Afya inaeendelea kuimarisha upatikanaji wa dawa na bidhaa nyingine za afya, Upatikanaji wa Huduma za Ubingwa na ubingwa Bobezi nchini,  kuimarisha huduma za Uchunguzi wa magonjwa ikiwemo huduma za Mionzi, kuimarisha Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto, kudhibiti maambukizi ya HIV/UKIMWI,  kifua kIkuu, malaria na magonjwa ya mlipuko, Ajira kwa watumishi na ufadhili wa wanafunzi katika ngazi na fani mbalimbali pamoja na kupitishwa kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote." amesema Waziri Ummy.


Amesema kuwa,  uwekezaji mkubwa uliofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  katika kuimarisha huduma ubingwa na ubingwa bobezi umewezesha wananchi wengi kupata huduma hizi ndani ya nchi kwa gharama nafuu badala ya kuzitafuta nje ya nchi.


Hata hivyo, amesema uwekezaji huu umeweza kuvutia wagonjwa mbalimbali kutoka nje ya nchi  na hivyo kuifanya Tanzania kuwa Kituo cha Tiba Utalii kwa ukanda wa nchi za afrika mashariki na kusini mwa Afrika.


Ameongeza kuwa kwa kipindi hicho cha miaka mitatu vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka  kutoka vituo 8,549 mwaka 2021 hadi kufikia vituo 9,610 Machi 2024 ikiwa  ni sawa na ongezeko la vituo 1,061.


"Serikali ya awamu ya sita imejenga na kufanya maboresho ya miundombinu ya kutolea huduma za afya ikiwa ni pamoja na ujenzi wa majengo mapya, ukarabati na kukamilisha ujenzi wa hospitali mpya katika mikoa mipya mitano, maboresho hayo yamegharimu jumla ya Shilingi Trilioni 1.02."amesema Waziri Ummy na kuongeza kuwa,


kutolea huduma za afya ikiwa ni pamoja na ujenzi wa majengo mapya, ukarabati na kukamilisha ujenzi wa hospitali mpya katika mikoa mipya mitano. Maboresho hayo yamegharimu jumla ya Shilingi Trilioni 1.02." amesema Waziri Ummy na kuongeza kuwa,


"Upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi umehakikisha kila mwananchi anapata mahitaji yote muhimu ya msingi ya kimatibabu pale anapoenda kupata huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya."


Sambamba na hayo amesema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hasssan katika kuimarisha ubora wa huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto kupitia Viashiria vikuu vinavyotumika kupima mwenendo wa ubora wa huduma kwa Nchi Wanachama wa Shirika la Afya Duniani imejidhihirisha wazi kuwa Tanzania imefanya vizuri katika kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto katika kipindi cha miaka mitatu.


Amesema kuwa, Serikali inaendelea kuajiri wataalam katika Sekta ya  Afya ambapo jumla ya wataalam 35,450 wa kada mbalimbali wameajiriwa na kusambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2023 hivyo kufanya, jumla ya ajira za mikataba kwa watumishi wa Afya 2,836 kupitia miradi mbalimbali ya Serikali zilitolewa.


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »