WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA KWANZA CHA MAANDALIZI YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

January 15, 2024

 WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, leo Januari 15, 2024 ameongoza kikao cha kwanza cha kamati hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip, Uwanja wa Ndege Zanzibar.


Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulah ambaye ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati hiyo.

Viongozi wengine waliohudhuria ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida pamoja na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Mipango, Bw. Lawrence Mafuru.





Share this

Related Posts

Previous
Next Post »