KATIBU MWENEZI CCM PAUL MAKONDA AHIMIZA WATANZANIA KUIPENDA NCHI YAO KWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

January 25, 2024






*Atoa rai kwa Watanzania kutotoa maneno ya kulaani Nchi kwani kufanya hivyo ni kujinyima mafanikio katika Nchi uishiyo._

“Tuna kila sababu ya kuipenda Tanzania, ndio nchi yetu, hazina yetu, urithi wetu na ndio mpango wa Mungu wetu kuwepo hapa lazima tuendelee kuimarisha Amani na Utulivu wetu”

“Watu wengi wanapenda kulaani nchi yao lakini mimi niwasihi isije ikatokea jambo ukaanza kutamka maneno ya laana kwasababu hautafanikiwa kwenye nchi uliyoilaani”

“Ukikasilishwa na mtu usitoe neno la kulaani Taifa lako kwakuwa Taifa hili ndio litabeba watoto wa watoto wako kama sio wewe basi watakula neema watoto zako na kama sio watoto zako basi wajukuu zako”

“Kwahiyo tuendelee kuliombea Taifa letu na Rais Samia na tunaposema tumuombee Rais wetu na Viongozi wetu watu wengi wanahitaji tunataka kuwaombea nini, we fikiria kama sio Utulivu, Msaada, Upendo wa Rais Dkt. Samia leo hii kungekuwa na maridhiano? na haya yote anaendelea kuyafanya kwa kuzingatia kanuni yake ya 4R ? Ndio maana tunasema tumuombee”

Makonda ameyasema hayo wakati akiwahutubia wana CCM na wanamchi wa Babati mkoani Manyara akiwa katika Diary yake ya kuhamasisha uhai wa Chama cha Mapinduzi na utlfuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi inayoendelea katika mikoa 20 ya Tanzania.

    

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »