RAIS WA UJERUMANI KUKUTANA NA FAMILIA ZA MASHUJAA WA VITA YA MAJIAMAJI

November 01, 2023

 



Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Dkt. Frank Walter Steinmeier Novemba 1, 2023 amewasili Uwanja wa Ndege wa Songea Mkoani Ruvuma kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani hapo.

Rais Mhe. Dkt. Steinmeier amepokelewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Songea Mjini Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, Viongozi wa Serikali pamoja na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma.

Akiwa mkoani hapo Mhe. Steinmeier atatembelea Makumbusho ya Mashujaa waliopigana vita ya Majiamaji pamoja na kukutana na familia za waliopigana vita hiyo.

       

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »