PROFESA JAMAL ATOA SHULE KUHUSU MABADILIKO YA TABIA NCHI

November 01, 2023

 

John Bukuku


Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Prof. Jamal Katundu amesema ongezeko kubwa la watu na kukua kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi hapa nchini linatarajiwa ama linatishia kupunguza kiwango cha upatikanaji wa maji kwa mtu na kufikia mita za ujazo 883 ifikapo mwaka 2035.
Amesema hayo wakati wa warsha ya wadau kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na ustahimilivu katika maeneo ya nchi.
Prof. Jamal amesema hali hiyo inaweza kuwa mbaya zaidi kwa maeneo kame ya nchi kama hakutakuwa na mikakati mathubuti ya kukabiliana na tabianchi

Amesema kwa mkoa wa Dodoma ambao ni makao makuu ya nchi, kustawi kwa kuongezeka kwa idadi ya watu na kukua kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi na za kijamii kumeisukuma Wizara ya Maji kuendelea na utekelezaji wa mipango mbalimbali ili kuwezesha upatikanaji wa vyanzo vya maji safi.

Prof. Jamal amepongeza watekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na ustahimilivu katika nyanda kavu za kitropiki kupiitia Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Wizara ya Maji
Utekelezaji wa mradi utawawezesha kuunganisha wataalam wa Wizara ya Maji kupitia kituo Mahiri cha Rasilimali za Maji na watafiti wabobezi kutoka SUA, na nchi za Uingereza, India na Niger.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »