TCRA :WANANCHI EPUKENI KUSAMBAZA TAARIFA ZISIZO NA UHAKIKA NA ZA UCHOCHEZI

October 26, 2023

 



Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt.Jabir Kuwe Bakari akitoa Muhtasari wa mwenendo wa Sekta ya Mawasiliano katika kipindi cha Julai hadi Septemba leo 25 Oktoba 2023 Jijini Arusha


Na.Vero Ignatus,Arusha

Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imefanya ufuatiliaji wa maudhui ya redio/ televisheni ambapo watoa huduma 80 walikutwa na makosa ya urushwaji wa maudhui yasiyofaa.

Akitoa mwenendo wa sekta ya mawasiliano katika kipindi cha Julai-septemba 2023 kwa waandishi wa habari leo Jijini Arusha Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt.Jabir Kuwe Bakari alisema tayari hatua za kisheria zimechukuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kupewa onyo, adhabu na maelekezo kwa kujibu wa sheria.

Dkt.Kuwe amesema TCRA kwa kushirikiana na Wizara ya maendeleo ya Jamii Jinsia wanawake na watoto na makundi maalum, imekamilisha uratibu wa programu maalum ya kuandaa vipindi vya maadili vitakavyorushwa na vituo vya utangazaji 150 vyenye leseni ya kiwilaya kwa lengo la kutoa elimu na kujenga jamii inayozingatia maadili, mila, desturi na utamaduni wa Mtanzania.

Sambamba na hayo TCRA imewakumbusha wananchi kuepuka kusambaza taarifa zozote zile zisizokuwa na uhakika na za uchochezi,kutambua na kiripoti kuhusu udanganyifu mtandaoni,na endapo yeyote akipokea ujumbe wa kitapeli au simu ya kitapeli atume ujumbe kwenda namba 15040.

Aidha TCRA imeendelea kuwasisitiza wananchi upatikanaji wa leseni za kidijitali kupitia mfumo wa Tanzanite Portal ,pamoja na kuhakikisha kuwa watumiaji hao wa huduma za mawasiliano kutoka TCRA ili kuendelea kuwa salama kupata huduma bora

Vilevile katika sekta ya Utangazaji zinaonyesha kuwa visimbizi 3,631,649 vilikuwa hewani hadi mwezi septemba 2023 ikilinganishwa na visimbizi 3,342,626 kwa.mwezi juni 2023 ambapo kati ya hivyo 1,789,090 ni vya dijitali kwa mfumo wa televisheni wa utangazaji wa mitambo ya ardhini na 1,846,559 ni vya mfumo wa televisheni wa setilaiti ambapo Dar inaongoza kuwa na visimbizi 1,390,163 ikifiatiwa na Arusha (287,908) mwanza 282,779 na mbeya (229,570) mikoa yenye visimbuzi vichache kuliko yote ni Manyara( 1,816)


'' Septemba 2023 kulikuwa na laini za simu milioni 67.12 kutoka milion 64.01 mwezi juni 2023 sawa na ongezeko.la 4.86%

kuanzia mwezi julai hadi septemba 2023 simu zilizobainika kuhusika na viashiria vya ulaghai au uhalifu ni 23,328 ikilinganishwa na 23,234 kati ya mwezi April hadi Juni 2023.

Akielezea juu ya sekta za kifedha kupitia mitandao ya simu amesema Tanzania inazidi kiendeleza mfumo jumuishi wa kifedha kutokana na ongezeko kwa watumiaji wa simu za mkononi .

"Takwimu za robo ya kwanza 2023/24 zinaonyesha kuwa huduma za kipesankupitia simu za mkononi zimeongezeka kutoka akaunti 47,275,660 mwezi june 2023 hadi kufikia 51,369,347 kwa mwezi Septemba 2023,ikiwa ni ongezeko la asilimia 8.7%ambapo miamala. Ya kifedha imeongezeka kutoka 420,675,884 kwa kipindi kilichoisha mwezi june 2023 hadi miamala 422,390,546 kufikia septemba 2023"

Dkt. Jabir.amesisitiza umuhimu wa taarifa ya takwimu za. Mawasiliano ni pamoja miongoni mwa faida zake ni kusaidia umma kupata taarifa, kuonyesha maeneo ya fursa mpya kwa wajasiriyamali, kiwasaidia watoa huduma kuweza kuboresha huduma zao, pamoja na kiwawezesha watendaji kichukua hatua stahiki kwenye maeneo ya kufanya iwezeshajj wenye tija katika sekta ya mawasiliano.

Aidha TCRA inatoa rasilimali za mawasiliano bure kwa wabunifu mbalimbali wanaohitaji kufanya majaribio kwenye huduma zao kwa kipindi maalum, kwani mwezi juni 2023 jumla ya wabunifu 4 walipewa rasilimali namba, ambapo hadi kufikia septemba 2923 imetoa rasilimali kwa wabunifu waoatao 9katika namba na. Mmoja ni katika masafa,.

Pamoja na hayo takwimu za watumiaji wa huduma za intaneti zinaonyesha kuendelea kuongezeka kwa watumiaji 1.24% kutoka kwa watumiaji 34,047,407 kwa mwezi juni 2023 hadi kufikia 34,469,022 mwezi septemba 2023.

"Baadhi ya sababu zinazochangia ongezeko hilo la matumizi ya Intaneti ninuwepo wa maudhui ya Kiswahili kwenye matandao wa ikijumuisha kuongezeka kwa programu -tumizi kwa lugha ya kiswahili.

Vilevile katika Sekta ndogo ya Posta katika kipindi cha mwezi julai hadi septemba 2023 vipeto 107,147 kutoka nje ya nchi ambapo huduma hiyo inaendelea kuchagiza ukuaji wa biashara mtandao.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »