Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (katikati), akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Namibia Mhe. Peter Katjavivi (kushoto) pamoja na Spika wa Bunge la Zambia Mhe. Nelly Mutti (kulia) wakati walipokutana katika Ofisi ndogo za Bunge la Angola wakati wa Mkutano wa 147 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ukiendelea nchini humo leo tarehe 23 Oktoba, 2023
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 23 Oktoba, 2023 akizungumza na Wajumbe wa kundi la Latini na Amerika kusini katika ukumbi mdogo wa Bunge la Angola wakati wa Mkutano wa 147 wa IPU akiwaomba wampigie kura katika Uchaguzi wa Urais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 nchini humo.