SPIKA WA BUNGE DKT. TULIA ACKSON ATEMBELEA BANDA LA WCF NANENANE MBEYA

August 05, 2023


 

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MBEYA

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), ametembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF) kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Tanzania kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya leo Agosti 4, 2023.

Mhe. Dkt. Ackson ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, alipata fursa ya kupewa elimu ya Fidia kwa Wafanyakazi iliyokuwa ikitolewa na Afisa Mfawidhi WCF, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bi. Rose Satta.

Alijulishwa kuwa WCF inatoa fidia endapo mfanyakazi ataumia au kuugua kutokana na kazi na endapo atafariki basi wategemezi wake watalipwa fidia.

Pia alielezwa kuwa Mfuko uliundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263 marejeo ya mwaka 2015] na inahusu waajiri na waajiriwa wote kutoka sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara.

Aidha Mhe, Spika alielezwa kuwa Mfuko unatoa jumla ya Mafao saba ambayo ni pamoja na Huduma ya matibabu, Malipo ya ulemavu wa muda, Malipo ya ulemavu wa kudumu, Malipo kwa anayemhudumia mgonjwa, Huduma za utengemao, Msaada wa mazishi na Malipo kwa wategemezi endapo mfanyakazi atafariki.

Maonesho ya mwaka huu ambayo yalifunguliwa rasmi Agosti Mosi, 2023 na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, yamewaleta pamoja washiriki kutoka nchi zinazofikia 30, kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera na yamebeba kaulimbiu isemayo “Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mfumo Endelevu wa Chakula”

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akionyesha furaha baada ya kupata elimu ya fidia alipotembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Tanzania kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya Agosti 4, 2023.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akisikiliza kwa makini kuhusu elimu ya fidia kwa wafanyakazi iliyokuwa ikitoelwa na Afisa Mfawidhi WCF, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bi. Rose Satta 
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akisikiliza kwa makini kuhusu elimu ya fidia kwa wafanyakazi. 
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), katikati, akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa WCF.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), katikati, akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa WCF.

 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »