NIC Yatunukiwa Cheti Cha Superbrand Kwa Mafanikio Sekta Ya Bima Nchini Tanzania.

August 14, 2023

 Katika jitihada za kutambua ufanis na utoaji wa huduma bora katika sekta ya bima nchini, Shirika la Bima la Taifa, NIC, imepokea cheti cha ubora kutoka kwa taasisi ya Superbrands kuwa kinara katika sekta hiyo ikiwa ni baada ya kufanyika kwa utafiti na tathmini ya kina ya huduma zake. Heshima ya kipekee ni uthibitisho kujizatiti imara kwa NIC katika weledi, ubunifu, na utoaji wa bidhaa na huduma za bima za ubora wa hali ya juu kuwahudumia Watanzania nchini kote.


Kutambuliwa kwa NIC na Superbrand kunaonesha namna kampuni ilivyojikita katika kuboresha viwangu vya juu vya ubora, kuwajali wateja, na kuzingatia weledi. Tukio hili si mafanikio tu kwa NIC, bali inaonyesha jitihada za makusudi na mchango wa pamoja unaonyeshwa na wafanyakazi, washirika, na wadau wote.

Shirika la bima la Taifa, NIC, kwa muda mrefu linajiendesha kama kinara katika soko la huduma za hisa nchini, likihudumia mahitaji ya wateja kwa kuwapatia huduma tofauti za bima ambazo zinalinda Maisha, mali, na biashara zao. Cheti hiki cha kutambuliwa na Superbrands, kinaiweka NIC kwenye nafasi ya kuwa shirika linaloaminiwa na mtoaji wa huduma endelevu za bima, na kuonyesha kujizatiti kwakwe kuhakikisha usalama katika masuala ya kifedha na kuwapatia utulivu wa akili kwa wateja wake.

Mkurugenzi Mtendaji wa NIC, Dkt. Elirehema Doriye ameonyesha furaha yake kwa mafanikio ya kutambuliwa na cheti hiki cha heshima kwa kusema kuwa, “ni heshima kubwa kupokea cheti cha utambulisho kutoka kwa taasisi ya Superbrand. Kutambuliwa huku ni uthibitisho wa kazi kubwa tunayoifanya Pamoja na kujitolea kwa kila mfanyakazi wa NIC, na inatuongezea chachu zaidi ya kuendelea kuboresha viwango vya huduma katika ya bima Tanzania.”

Kujitolea kwa NIC katika shughuli zake kwa kuzingatia weledi ni wa namna ya kipekee. Shirika limejizatiti kuendelea kuleta maendeleo chanya kwa jamii na kuchangia kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi kwa maendeleo ya Tanzania. Kutambuliwa na Superbrand kumekuja wakati sahihi na kuongeza ari zaid ya NIC kuendeleza ubora wa viwango vya hali ya juu, kutumia ubunifu na teknolojia ili kuwapatia wateja huduma wanazohitaji na kusaidia sekta nzima kusonga mbele zaidi.

Wakati NIC ikisonga mbele, pia inaipokea heshima ya cheti hiki cha ubora kama changamoto ya kuwa bora zaidi na kuendelea kutoa huduma za kipekee, kuborasha ubunifu, na kuchangia maendelea chanya kwa ukuaji na ustawi wa Tanzania.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa, NIC, Dkt. Elirehema Doriye (kulia) akiwa anapokea cheti cha kutambuliwa kwa huduma na bidhaa bora kutoka kwa Mkurugenzi wa Ukanda wa Afrika Mashariki Miradi ya Superbrands Bwana Jawad Jaffer (kushoto) wakati wa hafla wa utoaji wav yeti iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency the Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Ni mara ya kwanza NIC kutambuliwa na taasisi ya Superbrands kama kinara katika utoaji wa huduma na bidhaa za bima kwa sekta hiyo nchini.






Share this

Related Posts

Previous
Next Post »