.jpg)

.jpg)
AFISA Masoko Mwandamizi wa TASAC Martha Kelvin akimuonyesha mmoja wa watumiaji wa vyombo vya majini namna ya kuvaa jaketi okozi

.jpg)
.jpg)


| 
 | 
Na Mwandishi Wetu,Morogoro
SHIRIKA
 la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imetoa elimu ya Usalama, ulinzi na 
utunzaji wa mazingira mkoani Morogoro pamoja na kuendesha zoezi la 
ukaguzi wa Vyombo vya usafiri majini.
Ukaguzi
 huo ni sehemu mikakati ya Shirika hilo kuhakikisha vyombo vya usafiri 
majini vinakuwa na ubora unaotakiwa kwa kuzingatia viwango. 
Zoezi
 hilo liliendeshwa na Maafisa Ukaguzi na Udhibiti wa Vyombo vya Majini  
wa Shirika hilo, Bw. Gabriel Manase na Maulid Nsalamba katika wilaya ya 
Ifakara mkoani humo. Maafisa hao walitoa elimu ya usalama na ulinzi 
ikiwemo utunzaji wa mazingira wanapokuwa kwenye shughuli zao
Akizungumza
 wakati wa zoezi hilo Manase alisema elimu hiyo ina umuhimu mkubwa sana 
hivyo jamii inapaswa kuitambua na kuweza kuzuzungatia wakati wote 
wanapotekeleza shughuli zao za kila siku.
Zoezi
 hili lilianza tarehe 11 Novemba, 2022 ifakara katika maeneo ya 
Ngalimila, Ngapemba, Utengule, Chita na Mngeta na Mchombe na litaendelea
 katika mikoa ya  iringa na Dodoma lengo ni kuhakikisha jamii inapata 
elimu.
Zoezi
 hilo liliendeshwa pia kwa ushirkiano na Afisa Masoko Mwandamizi wa 
TASAC Martha Kelvin na Afisa Uhusiano Mwandamizi Amina Miruko ambapo 
waliitaka jamii kuhakikisha inazingatia usalama kwenye vyombo vya maji 
ili kuweza kuepukana na ajali ambazo zinazaweza kuwakuta wawapo 
safarini.

EmoticonEmoticon