RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA KIDATU –IFAKARA YENYE KM 66.9 PAMOJA NA DARAJA LA MTO RUAHA KATIKA ENEO LA NYANDEO KIDATU

May 04, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe pamoja Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy kushoto na Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer kulia kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 katika sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Nyandeo Kidatu mkoani Morogoro. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli watatu kutoka kushoto pamoja viongozi mbalimbali na wabunge wa mkoa wa Morogoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy mara baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 katika sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Nyandeo Kidatu mkoani Morogoro
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi pamoja na viongozi wengine wakiwemo Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy anayevuta utepe, Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer pamoja na wabunge mbalimbali wa mkoa wa Morogoro
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la Ruaha lenye urefu wa mita 130.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa kidatu kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la kidatu lenye urefu wa mita 130.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mkuu wa mkoa wa Morogoro Steven Kebwe kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la mto Ruaha lenye urefu wa mita 130.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa kidatu kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la kidatu lenye urefu wa mita 130.


Mbunge wa Mikumi Joseph Haule akitumbuiza mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la mto Ruaha lenye urefu wa mita 130.
Wananchi waliohudhuria katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la mto Ruaha lenye urefu wa mita 130.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kwa njia ya simu ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo kuhusu matatizo ya mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa maji katika kata ya Kidodi mkoani Morogoro.

- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kidodi wakati akielekea Kidatu mkoani Morogoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumzana wananchi wa Kidodi wakati akielekea Kidatu mkoani Morogoro.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »