WAZIRI MPINA ATOA MAAGIZO KWA KATIBU MKUU MIFUGO YANAYOTAKIWA KUTEKELEZWA NDANI YA WIKI MBILI

February 25, 2018

Katika Picha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina na ujumbe wake akiwa akiwa katika ziara katika kituo cha Taifa cha uzalishaji Mbegu bora za Mifugo kwa njia ya chupa, (NAIC) kilichopo Mjini Arusha.

 
Katikati Katibu Mkuu Mifugo Dkt. Maria Mashingo akisoma Hotuba katika zoezi la uzinduzi wa madume ya kisasa ya mbegu bora za Ng’ombe katika kituo cha taifa cha uzalishaji mbegu bora kilichopo mjini Arusha, Kushoto ni waziri wa Mfugo na Uvuvu Mhe. Luhaga Mpina, na kulia ni Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko  wa Wizara hiyo, Dkt.Lowlence Asiimwe.
 
Katikati Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akiangalia dume bora la kisasa kutoka nchi ya New Zealand katika kituo cha Taifa cha Uhimilishaji cha (NAIC) Arusha jana alipokuwa katika ziara maalum ya uzinduzi wa Madume hayo.kulia ni  Dkt Paul Mollel, Mkurugenzi wa Kituo hicho.
Katika Picha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akikata utepe kuashiria uzinduzi wa madume bora ya kisasa kutoka nchi ya South Africa na New Zealand  yaliyoletwa nchini kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu bora za mifugo. Pembeni yake ni katibu Mkuu Mifugo Dkt  Maria Mashingo na ujumbe wake.
NA, MWANDISHI MAALUM - ARUMERU
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepewa wiki mbili  kufanya tathmini kuona kama kuna haja ya kuagiza maziwa na mazao yake kutoka nje ya nchi na kama waagizaji wanafuata taratibu na masharti ya kisheria yaliyowekwa na Serikali.
Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina alipokuwa katika ziara ya kutembelea kituo cha Taifa za uzalishaji wa mbegu Bora za Mifugo kwa njia ya chupa kilichopo Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.
Waziri Mpina pia aliitaka Wizara yake kuandaa mpango kazi utakao wezesha kuzalisha Ng’ombe milioni moja kwa mwaka  kuanzia mwaka wa fedha 2018/19 ili kuweza kusaidia kujenga viwanda vya maziwa na  kuweza kumudu soko la ndani  na hata kuhudumia bara zima la Afrika  na kusaidia kuongeza pato la Taifa.
“Kuna makampuni 43 nchini yanayoingiza maziwa toka nje ya nchi,na makampuni 81 yanayojishughulisha na maziwa na mazao yake,Wizara ifanye tathmini kama kweli tunahitaji kuingiza maziwa hayo. Alisisitiza Mpina.”
Aliongeza kuwa maziwa mengi yanaingia ndani ya nchi kwa kupitia njia za panya, na kusema kuwa wale wote wanaojishughulisha na biashara hizo wapo hatarini kukamatwa na sheria itachukua mkondo wake. “Mimi na Wizara na yangu tumejipanga kimwili kiroho na kiakili tutawashughulikia wote wanaofanya biashara hizi kimagendo hakuna suluhu kwa yeyote atakaye kamwatwa. Alisisitiza.”
Sambamba na hilo, Waziri Mpina pia alimpongeza katibu Mkuu Mifugo Dkt Maria Mashingo kwa kazi kubwa ya kuhakikisha kuna kuwepo na mbegu za kutosha kwa kuwepo kwa madume bora 26 hadi sasa yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya dozi 3,120,000 kwa mwaka.
Kwa upande wake, Dkt. Mashingo alimshukuru Waziri kwa kutoa maelekezo ambayo yanalenga kuleta mapinduzi ya mifugo na kwamba ameyapokea na yatatekelezwa  mara moja kama alivyoagiza.


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »