WACHUUZI WA NAZI SOKO LA MGANDINI WAELEZA SABABU ZA BIDHAA ZINAZOTOKA MOMBASA KUKUBALIKA

February 27, 2018
Chama cha wauza nazi katika soko la Mgandini Jijini Tanga wameeleza sababu za nazi zinazotoka Mombasa nchini Kenya kukukabilia kuliko za Tanga kutokana na ubora zilizokuwa nazo na kubwa.

Hayo yalibainishwa na Katibu wa chama cha Wauza Nazi katika soko hilo (Coconut Group) Kassim Mohamed katika mahojiano na Blog hii ambapo alisema sababu nyengine ni wakulima nchini humo kuiweka nazi hiyo muda mrefu shambani kwa kufuata utaratibu kuliko ilivyo kwa wengine.

Alisema hali hiyo imezifanya nazi zinazotoka huku kuonekana kupendwa na wafanyabiashara wengi ambao wamekuwa wakifika kwa ajili ya ununuaji wa zao hilo kwenye soko hilo kuliko ilivyo za mkoani Tanga hali inayotajwa kuchangiwa na wakulima.

“Kwa mfano utakuwa mkulima wa nazi mkoani Tanga anavuna nazi mapema shambani kutokana na shida alizokuwa nazo lakini wa Mombasa nchinio Kenya wamekuwa wakiziweka muda mrefu na hivyo zinavunwa zinakuwa kubwa na wenye ubora”Alisema

“Lakini pia wanasema uharakishaji wa uvunaji wakulima hao zao hilo wamepeleka kupata nazi ndogo ambazo sokoni zimekuwa na changamoto kubwa kuliko ambazo zinatoka nchi jirani ya Kenya kwani hizi za Tanga unaweza kuwa nazo unauza reja reja “Alisema.

Alisema sababu inayopelekea wakulima hao kupata nazi ndogo inatokana na kushindwa kuendeleza zao hilo kwa kuipanda mingine kwani iliyopo hivi sasa ni ya zamani ambayo wamerithi katika maeneo yao.


“Lazima watambue kuwa hata kama utakuwa umerithi mnazi unapaswa kutambua umuhimu wa kupanda mingine kwani inapokaa muda mrefu inapelekea kuzalisha nazi ndogo.

Naye mchuuzi kwenye soko hilo,Akida Juma aliwataka wakulima wa zao hilo mkoani hapa kubadilika kwa kulima kisasa ili kuondokana na kutegemea minazi ya zamani ili waweze kuvuna jambo ambalo linaweza kuwapeleka kukosa soko kabisa kutokana na ushindani uliopo.

“Ndugu zangu tunajua minazi mingi watu wamerithi kutoka na kupandwa miaka ya nyuma hivyo hakikisheni mnaipanda mingine kwa kufuata taratibu mzuri na baadae mnaweza kupata mafanikio kuliko sasa “Alisema.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »