MZUNGUKO
WA NNE KOMBE LA SHIRIKISHO LA AZAM KUENDELEA WIKIENDI HII
Hatua ya mzunguko wa Nne(4) wa mashindano ya Kombe la
Shirikisho la Azam inaendelea Jumamosi Februari 24, 2018 kwa michezo miwili.
Singida United watakuwa Uwanja wa Namfua Mjini Singida
kucheza na Polisi Tanzania saa 10 jioni na mchezo mwingine utakaohitimisha siku
hiyo utakuwa kati ya KMC watakaokuwa nyumbani Azam Complex,Chamazi
kuwakaribisha Azam FC saa 1 usiku.
Mzunguko huo wa Nne(4) utaendelea tena Jumapili Februari
25, 2018 kwa Buseresere kuwaalika Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Nyamagana
Mwanza mchezo utakaochezwa saa 8 mchana wakati Majimaji FC ya Ruvuma watakuwa
nyumbani kwenye uwanja wa Majimaji kuwakaribisha Young Africans ya Dar es
Salaam mchezo ukichezwa saa 10 jioni nao Ndanda FC watakuwa ugenini kucheza na
JKT Tanzania Azam Complex Chamazi saa 1 usiku.
Mzunguko huwa wa 4 utakamilika Jumatatu Februari 26, 2018 Kiluvya
United dhidi ya Tanzania Prisons saa 8 mchana Uwanja wa Mabatini na Stand
United watawaalika Dodoma FC saa 10 jioni uwanja wa Kambarage.
LIGI
KUU YA WANAWAKE YA SERENGETI PREMIUM LITE KUZINDULIWA RASMI NA WAZIRI MWAKYEMBE
JUMAPILI
Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Premium Lite hatua ya
Nane bora inataraji kuzinduliwa rasmi mkoani Kigoma Jumapili Februari 25,2018
kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika.
Mchezo utakaotumiwa kuzindua ligi hiyo utazikutanisha timu
za Kigoma Sisterz ya Kigoma dhidi ya Simba ya Dar es Salaam.
Aidha uzinduzi utaenda sanjari na mpango maalumu wa FIFA
wa kuhamasisha soka la Wanawake uliopewa jina la Live Your Goal ambapo mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dr.Harrison
Mwakyembe.
Mbali na mechi ya uzinduzi mechi nyingine za ligi hiyo ya
Wanawake ya Serengeti Premium Lite zinatarajia kuchezwa kesho kwenye viwanja
tofauti.
Uwanja wa Samora Panama FC watacheza dhidi ya Evergreen
Queens ya Dar es Salaam saa 10 jioni,huko Mbweni JKT Queens watacheza dhidi ya
Alliance saa 10 jioni,mabingwa watetezi Mlandizi Queens wanasafiri mpaka
Jamhuri Dodoma kucheza na Baobab Queens.
Wakati
huohuo Kozi ya makocha wa kozi ya grassroots kwa watoto wenye
umri wa miaka 6-12 Wasichana na Wavulana imeanza Jumatano kwenye Uwanja wa Lake
Tanganyika,Ujiji,Kigoma.
MCHEZO
WA LIPULI NA NDANDA WASOGEZWA
Bodi ya Ligi (TPLB) imefanya mabadiliko ya mchezo namba
153 kati ya Lipuli na Ndanda uliokuwa uchezwe Ijumaa Machi 2,2018 kwenye Uwanja
wa Samora,Iringa.
Mchezo huo sasa umesogezwa mpaka Jumapili Machi 4,2018 na
utachezwa kwenye Uwanja ule ule wa Samora.
Sababu za kusogezwa mbele kwa mchezo huo ni kuipa nafasi
Ndanda FC kusafiri kutoka Mtwara baada ya mchezo wao na Yanga ambao sasa
umepangwa kuchezwa Jumatano Februari 28 ,2018 kwenye Uwanja wa Nangwana Sijaona
,Mtwara.
IMETOLEWA
NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA TFF