MFUKO WA UDHAMINI WA MIKOPO BOT WAONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUKUZA BIASHARA NA UCHUMI

February 06, 2018
 Bibi Fatuma Kimario, Meneja Msaidizi Idara ya Kudhamini Mikopo, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), akitoa mada juu ya Mfuko huo unavyofanya kazi kwenye semina ya waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha inayofanyika mkoani Mtwara Februari 5, 2018.

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
KIASI cha Shilingi trilioni 1.30 kimetolewa kama dhamana ya mkopo chini ya uchamini wa Mfuko wa Udhamini wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT) kwa taasisi 87 zinazojishughulisha na kuuza mazao nje ya nchi, (ECGS) na Sekta ya Wajasiriamali wadogo na wakati (SME-CGS), Meneja Msaidizi Idara ya Kudhamini Mikopo ya benki hiyo Bibi. Fatma Kimario amesema.
Akiwasilisha mada kwenye semina ya  waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha, inayoendelea mjini Mtwara, Februari 5, 2018 Bibi Kimario alisema, kupitia  Mfuko wa Udhamini wa Mauzo nje ya Nchi (ECGS), na Sekta ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati, (SME-CGS) udhamini huo ni wa mkopo wa fedha wa kiasi cha shilingi trilioni 1.70 zilizotolewa na taasisi za fedha ili  kukopesha wanufaika hao.
Akifafanua zaidi Bibi Kimario alisema, “Sekta zilizonufaika chini ya Mfuko wa kudhamini Mauzo nje ya nchi (ECGS) ni 21 ambapo taasisi za fedha zilitoa mikopo kwa sekta 21 ambazo ni pamoja na Kilimo, Viwanda, Uchimbaji na Uvuvi ambazo kwa ujumla wake zilipata mikopo ya jumla ya shilingi trilioni 1.65, ambapo Mfuko wa Udhamini ulitumia kiasi cha shilingi trilioni 1.25 kudhamini mkopo huo” Alifafanua.
Akifafanua zaidi, Mtaalamu huyo kutoka BoT, alisema, sekta ya Kilimo ndiyo iliyonufaika zaidi kwa kupata mkopo wa shilingi trilioni 1.52, Viwanda bilioni 101, Uchimbaji, shilingi bilioni 14 na  Uvuvi bilioni 4.5 .
Kwa upande wa Sekta ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati, (SME-CGS), taasisi 65 zilinufaika kwa kupata mkopo wa jumla ya shilingi bilioni 10.52 ambapo Mfuko ulitumia kiasi cha shilingi bilioni 5.14 kudhamini mkopo huo.
Akifafanua jinsi sekta hizo zilivyonufaika Bibi Kimario alisema “Sekta ya Kilimo ndiyo iliyoongoza kwa kupata mkopo wa shilingi bilioni 4.8, Viwanda bilioni 1.5, Ujenzi bilioni 1.4, Elimu milioni 930, Utalii milioni 874, Mawasiliono milioni 570, Huduma 130, Uchimbaji madini milioni 68, Afya milioni 63, Uvuvi milioni 50, na Uchukuzi milioni 34.” Alisema.
Bibi Kimario ameelezea utaratibu wa udhamini umekuwa wa mafanikio makubwa ambapo kwa kuongezeka kwa pato la Halmashauri ambazo vyama vya Ushirika vya Msingi vilivyodhaminiwa na mfuko huu.
Kuchangia ongezeko la fedha za kigeni kutokana na mauzo ya nje ya nchi kuchangia makusanyo ya kodi kwa serikali  zitokanazo na bidhaa za viwandani.
 Dkt.Suleiman Missango, Meneja Msaidizi Idara ya Utafiti Kurugenzi ya Sera za Uchumi na Utafiti BoT, akifafanua baadhi ya mambo yahusuyo utekelezaji wa majukumbu mbalimbali ya BoT.
 Baadhi ya washiriki wakifuatilia semina hiyo.
  Baadhi ya washiriki wakifuatilia semina hiyo.
 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Itifaki cha BoT, Bibi. Zalia Mbeo, (mbele) akiwa na wataalamu wa benki hiyo wakati wa semina hiyo.
 Bibi. Grace Aswile, Meneja Msaidizi-Idara ya Masoko ya Ndani ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), akiwasilisha mada kuhusu utaratibu wa kuendesha soko la dhamana za serikali ambapo pamoja na mambo mengine alisema, BoT inaendelea na uhamasishaji na elimu kwa umma wa watanzania wote kushiriki katika minada hii kama njia moja wapo ya kujiwekea akiba na kuchangia shughuli za uchumi wa nchi yetu.
 Bibi. Grace Aswile, Meneja Msaidizi-Idara ya Masoko ya Ndani ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), akiwasilisha mada kuhusu utaratibu wa kuendesha soko la dhamana za serikali
 Meneja Usimamizi wa Mabenki  wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT),  Bw. Eliamringi Mandari, akitoa mada kuhusu Kanuni mpya za maduka ya kubadilisha fedha yaani (Bureaux de change). chini ya kanuni hii wamiliki wanatakiwa kuonyesha viwango vya kubadilisha fedha sehemu ya uwazi na waonyeshe leseni ya BoT ikiwa ni pamoja na kutoa Fiscal receipt(EFDs) kwa wateja wao.
Meneja Msaidizi-Idara ya Uhusoano wa Umma na Itifaki, Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bi. Vicky Msina, (kushoto) akiwa na Bw.Sadiki Nyanzowa, ambaye ni Afisa Msaidizi-Idara ya Udhamini wa Mikopo BoT.

Afisa Uhusiano Mkuu kutoka Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki wa BoT, Bw. Lwaga Mwambande
-- Khalfan Said Photojournalist K-VIS MEDIA P.o.box 77807 Dar es Salaam, Tanzania Mobile: +255-784-646-453/+255-653-813-033 Blog: khalfansaid.blogspot.com

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »