JAFO AKERWA NA UTENDAJI MBOVU ROMBO

January 24, 2018
JAFO ROMBO (1)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akitoa maelekezo kwa watendaji wa Halmashauri ya Rombo
JAFO ROMBO (2)
Ujenzi wa jengo la upasuaji linaloendelea katika Kituo cha Afya Karume wilayani Rombo
JAFO ROMBO (3)
Nyumba ya daktari inayojengwa katika Kituo cha Afya Karume wilayani Rombo
JAFO ROMBO (4)
Jengo la wodi ya wazazi inayojengwa  katika kituo cha Afya Karume.
…………………………………………………………………………………………….
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ameonyesha kukerwa na kutoridhishwa na kasi ya utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo na watendaji wake wa chini kwa kushindwa kwenda sambamba na kasi anayoitaka katika kuwaletea wananchi maendeleo.
Hali hiyo ilijitokeza leo wakati Jafo alipokuwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo iliyopo mkoani Kilimanjaro.
Amesema Halmashauri ya wilaya ya Rombo ni miongoni mwa Halmashauri zilizopokea fedha za awamu ya kwanza ya uboreshaji vituo vya afya lakini licha ya kupokea fedha hizo tokea mwezi Agosti mwaka 2017 bado wapo nyuma ukilinganisha na halmashauri zingine zilizopata fedha kwa wakati mmoja.
Akikagua kituo cha afya Karume , Waziri Jafo amemtaka mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  kufanya kazi kwa weledi na kuwapa ushirikiano  wa kutosha watendaji walio chini yake ili waweze kumaliza kazi hiyo kabla Februari 25, mwaka huu.
Kadhalika, Jafo amewapongeza Mkuu wa wilaya ya Rombo Agness Hokololo na Katibu Tawala wake wa wilaya Asenga kwa kazi kubwa wanayofanya ya kusimamia maendeleo ya wilaya hiyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »