NA MWANDISHI WETU,HANDENI.
BASI la
kampuni ya Tahmed lililokuwa linafanya safari zake kati ya Dar es Salaam na
Arusha limewaka moto na kuungua katika eneo la Kitumbi Kata ya Kabuku wilayani
Handeni mkoani Tanga likiwa njiani huku akibiria wakinusufika baada ya kuwahi
kutoka nje.
Kamanda wa
Polisi mkoani Tanga,Edward Bukombe aliuambia Mtandao wa Tanga Raha kuwa tukio hilo
lilitokea leo saa nne na dakika arobaini na tano likiwa linaelekea mkoani
Arusha.
Alilitaja
gari hilo lenye namba za usajili T.483 DFL lilikuwa likiendeshwa na Bakari
Saidi (30) likiwa na abiria sita lilipofika eneo hilo ndipo lilipowaka moto
kutokana na hilifau za kiufundi .
Alisema
wakati basi hilo likianza kuwaka moto abiria waliokuwepo ndani waliwahi kutoka
na kujinusuru na kifo huku wakiliacha likiendelea kuungua moto .
Hata hivyo
Kamanda huyo alisema chanzo cha ajali hiyo bado wanafuatilia ili kuweza kubaini
moto huo ulisababishwa na nini.
“Labda nisema
taarifa ya kuungua moto na kuwaka basi hilo ni kweli kwa sasa tunafanya
uchunguzi kwa lengo la kubaini nini chanzo chake “Alisema.
Mwisho.