Serikali kupitia Waziri wa Maliasili na
Utalii Dk.Hamisi Kigwangalla ameunda Kamati ya Kitaifa ya kuandaa mwezi
maalum wa maadhimisho ya urithi wa Tanzania ambapo kamati hiyo
itajumuisha viongozi mbalimbali waandamizi wakiwemo wakuu wa Mikoa,
Mawaziri, Wakurugenzi na wakuu wengine wa Idara za Serikali na mashirika
binafsi.