_____________________________
Mchezaji Said Hamis Juma (Ndemla) amefanikiwa kufuzu kwenye majaribio yake ya kucheza Soka la kulipwa barani Ulaya.
Ndemla
aliyekuwa nchini Sweden kwa majaribio kwenye klabu ya Eskilstuna ya
huko.anatarajiwa kurejea nchini siku ya jumatatu inayokuja.
Na
mara baada ya kurejea. klabu za Simba na Eskilstuna zitaanza mazungumzo
ya kimkataba ili kumwezesha kiungo huyo kwenda Sweden kwa ajili ya
kucheza Soka huko.
Kiufupi
klabu imefurahishwa na azma ya Ndemla ya kutaka kusonga mbele zaidi, na
kama ilivyo desturi na utamaduni wa Simba, klabu haitasita kumruhusu
mchezaji yoyote anayepata fursa adhimu kama hiyo itakayomsaidia mchezaji
binafsi.klabu na Taifa kwa ujumla.
Wakati huo huo kesho klabu ya Simba itakutana na viongozi wote wa matawi.
Mkutano
huo ni maandalizi ya mkutano mkuu maalum wa klabu wa tarehe 3-12-2017.
na mkutano huo wa kesho utafanyika makao makuu ya klabu kuanzia saa Nne
kamili asubuhi ya jumapili ya tarehe 26-11-2017.
Mwisho
Uongozi
wenu unawaomba Wanachama na washabiki wa klabu yetu kujitokeza kwa
wingi kesho uwanja wa Uhuru kuishangilia timu yao, itakapocheza mchezo
wa ligi kuu dhidi ya Timu ya Lipuli ya Iringa.
Imetolewa na.....
HAJI S. MANARA
Mkuu wa Habari na mawasiliano Simba Sports Club.