TANGAZO KUTOKA TANGA UWASA KUTOKUWA NA HUDUMA YA MAJI

October 24, 2017

Kuna tatizo la Umeme Jiji lote l Tanga pamoja na  eneo la Mabayani na Mowe tangu saa 10:10 alfajiri ,hivyo pampu za kusukuma maji zimesimma na hakutakuwa na maji hadi umeme utakaporejea.

Shirika la Tanesco wanaendelea kushughulikia utatuzi wa tatizo hilo na Mtambo utaanza kufanya kazi umeme utakaporejea.

Huduma ya Maji itaimarika kwa awamu baada ya mtambo kuanza kufanya kazi hivyo tunaomba radhi kwa usumbufu unaoweza kujitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Mkurugenzi Kitengo cha Uhusiano Tanga UWASA.


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »