TUME YA UCHAGUZI YAMTEUA NDG. CATHERINE RUGE KUWA MBUNGE WA VITI MAALUM CHADEMA

May 04, 2017
 DSC_0428
KUHUSU UTEUZI WA CATHERINE NYAKAO RUGE KUWA MBUNGE WA VITI MAALUM KUPITIA
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
Kwa mujibu wa Ibara ya 78(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ikisomwa pamoja na Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kikaochake cha tarehe 04 Mei, 2017imemteuaNduguCatherine NyakaoRuge kuwa Mbunge wa VitiMaalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kujazanafasiiliyoachwawazi na Mhe. Dkt. Elly Marco Macha.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemteuaNduguCatherine NyakaoRuge baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa mujibu wa Kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343,alitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuweponafasiwazi ya Mbunge wa VitiMaalumkupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, baada ya aliyekuwaMbunge wa VitiMaalumMhe. Dkt. Elly Marko Macha kufariki dunia na hivyo kuwepo nafasi wazi.
Imetolewaleo tarehe 04 Mei, 2017 na:-
Kailima, R.K
MKURUGENZI WA UCHAGUZI

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »