Ile show ya redio ya vijana maarufu kama Shujaaz Radio Show ikiongozwa na DJ Tee,
wiki hii tarehe 20 itakuwa inaangalia matatizo yanayowakumbwa wasichana
kutokana na shule kuwa mbali na makazi yao hivyo kusababisha mafanikio
duni katika elimu ya wasichana nchini Tanzania.
"Kwa
sababu pia ni story inayozungumziwa sana hapa Bongo kwa sasa hasa suala
la sheria ya kumrudisha msichana shuleni baada ya kujifungua, tumeamua
kuungana kwa pamoja na vijana wengine kulizungumzia hili kwa kina."
alisema DJ Tee.
Shujaaz Radio Show
husikika kila Jumamosi kupitia vituo vitano vya redio nchini Tanzania,
vikiwemo East Africa Radio (saa tisa alasiri) na TBC FM (saa kumi na
moja jioni). Vituo vingine ni Abood FM ya Morogoro (saa nne asubuhi),
Chuchu FM ya Zanzibar (saa tisa alasiri) na Kings FM ya Njombe (saa kumi
jioni).