RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA CHA KABYAILE MISENYI MKOANI KAGERA

January 02, 2017


kag1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika eneo la Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kabyaile Misenyi Mkoani Kagera.
kag2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria kuanza kwa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kabyaile Misenyi Mkoani Kagera. Wengine katika picha ni Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage, Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Vija Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama pamoja na Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako wakiwa wameshika utepe huo.
kag3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Kituo cha Afya cha Kabyaile Misenyi Mkoani Kagera.
kag4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua maeneo ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua maeneo ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua maeneo ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag7 kag8
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika eneo la mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag9
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika eneo la mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag10
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika eneo la mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera.
kag11
Taaswira ya moja ya jengo katika mradi huo wa kituo cha Afya cha Kabyaile kilichopo Misenyi mkoani Kagera. PICHA NA IKULU
………………………………………………………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Jumapili Januari Mosi, 2017 ameendelea na ziara yake ya siku mbili Mkoani Kagera kwa kukagua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa kituo cha afya cha Kabyaile kilichopo Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera
Akizungumza na wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kituo hicho cha Afya Rais Dkt Magufuli amesema serikali kwa sasa imeweka nguvu kubwa katika kurejesha miundo mbinu ya huduma za jamii iliyoharibiwa na tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10,2016 Mkoani humo badala ya kujenga nyumba ya mwananchi mmoja mmoja.
”Na ndio maana nimeona leo hapa tarehe moja mwezi wa kwanza mwaka 2017 niwaeleze ukweli maana kuna watu wanapitapita huko na wapo wengine nyumba zao zilibomoka kidogo wakadanganywa wakaambiwa kuwa serikali itakuja kuwajengea nyumba wakazibomoa zote ”waafwa” kama ulitegemea ukiibomoa utalipwa fidia,hakuna”
Aidha Dkt Magufuli amemwagiza Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kupeleka huduma ya umeme katika kituo hicho cha afya alichokiwekea jiwe la msingi,ambapo pia ameahidi kutoa kiasi cha shilingi Bilioni moja kwa ajili kutengeneza barabara inayoelekea kituoni hapo kwa kiwango cha lami.
Pia ameuagiza uongozi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaojenga kituo hicho cha afya kuharakisha ujenzi wake na kukamilika kabla ya mwezi februari badala ya Machi mwaka huu.
Dkt Magufuli ameutaka uongozi na wananchi wa Wilaya ya Misenyi na maeneo mengine nchini kutumia vyema mvua chache zinazonyesha mkoani humo kulima mazao yanayokomaa kwa muda mfupi ili kuepukana na baa la njaa na kwamba serikali haina mpango wa kugawa chakula cha bure.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Kagera.
01 Januari, 2017

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »