Waziri
wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiongoza kikao
kilichoshirikisha Watendaji kutoka Benki ya Dunia pamoja na watendaji
kutoka Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake ikiwa ni pamoja
na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) na Wakala wa
Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA).
Mtendaji
Kutoka Benki ya Dunia anayeshughulikia mazingira Vladislav Vucetic,
akielezea mikakati ya benki hiyo katika ushirikiano wake na Serikali
ili kupanua sekta za nishati na madini.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (kushoto
waliokaa mbele) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
anayeshughulikia masuala ya Nishati Dkt. Juliana Pallangyo ( wa pili
kutoka kushoto waliokaa mbele) wakifuatilia kwa makini maelekezo
…………………………………………………………………………………………………….
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati na Madini
Profesa Sospeter Muhongo ameelezea mikakati ya Serikali katika
uboreshaji wa sekta za nishati na madini na kuongeza kuwa Serikali
ipo tayari kushirikiana na Benki ya Dunia (WB) katika uboreshaji wa
sekta hizo ili ziwe na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.
Profesa Muhongo aliyasema hayo
alipokutana na Watendaji kutoka Benki ya Dunia pamoja na watendaji
kutoka Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake ikiwa ni pamoja
na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) na Wakala wa
Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA)
Akizungumzia Sekta ya Nishati
nchini Profesa Muhongo alisema kuwa serikali imeweka mikakati mbalimbali
ya kuhakikisha kuwa Sekta ya nishati inakuwa na mchngo mkubwa katika
ukuaji wa uchumi na kutoka katika kundi la nchi masikini duniani na
kuingia katika kundi la nchi zenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025
kama Dira ya Maendeleo ya Taifa ifanvyofafanua
Aliongeza kuwa, Serikali kwa mara
ya kwanza imetenga asilimia 40 ya bajeti yake katika miradi ya
maendeleo ikiwa ni pamoja na ya umeme na kuendelea kufafanua kuwa
katika bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2016/17, Wizara imetenga
asilimia 94 ya bajeti yake katika miradi ya maendeleo, ambapo katika
Idara ya Nishati asilimia 98 itakwenda kwenye miradi ya umeme.
Waziri Muhongo alisema kuwa ili
kuimarisha Sekta ya Nishati, Wizara imepanga kupanua sekta ya nishati
kwa kukaribisha wawekezaji binafsi kuwekeza katika sekta ya uzalishaji
na uuzaji wa umeme pamoja na kuwapo kwa mwongozo utakaowawezesha
kuzalisha umeme.
Alindelea kusema kuwa Wizara
inatarajia kuimarisha usambazaji wa umeme vijijini kwa kushirikiana na
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na TANESCO.
Profesa Muhongo aliendelea kutaja
mikakati mingine kuwa ni pamoja na kuimarisha mradi wa usambazaji wa
umeme wenye msongo wa kilovolti 400 kupitia Iringa, Mbeya, Tunduma
hadi katika eneo la Kabwe nchini Zambia na kusisitiza kuwa upembuzi
yakinifu unatarajia kukamilika mapema Desemba mwaka huu kabla ya kuanza
kwa mradi.
Aliendelea kutaja miradi mingine
kuwa ni pamoja na mradi wa usambazaji umeme kupitia Mbeya, Sumbawanga,
Mpanda, Kigoma, Nyakanazi na kuiomba Benki ya Dunia kushirikiana na
Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ili kufanikisha mradi huo.
“Kuna mradi wa kuunganisha Tanzania na Uganda ujulikanao kwa jila la Tanzania – Uganda inter-connector unaounganisha Mwanza, Geita, Nyakanazi, Kyaka- Bukoba hadi Masaka nchini Uganda.
Akizungumzia Sekta ya Gesi
Profesa Muhongo alieleza kuwa serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha
nishati ya gesi inatumika ipasavyo katika uzalishaji umeme pamoja na
kusambazwa katika matumizi ya majumbani.
Aliongeza kuwa serikali imeweka
mikakati ya kusambaza gesi majumbani kwa ajili ya matumizi ya kupikia
katika mikoa ya Dar es salaam, Lindi, Mtwara na katika maeneo mengine
ya Pwani.
Akielezea Sekta ya Madini
Profesa Muhongo aliiomba Benki ya Dunia kusaidia katika ununuzi wa
vifaa vya madini kwa wachimbaji wadogo pamoja na katika kuwapatia
elimu kuhusu mazingira, uchenjuaji wa madini na kuongeza ajira
hususan katika maeneo ya madini yaliyopo vijijini
Naye Mtendaji Kutoka Benki ya
Dunia anayeshughulikia mazingira Vladislav Vucetic alisema Benki ya
Dunia ipo tayari kushirikiana na Serikali katika uendelezaji wa sekta
za nishati na madini ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.