MKUU WA MKOA WA MBEYA ASEMA SITAKI TAKWIMU ZA MADAWATI HEWA MKOA WA MBEYA

June 07, 2016

 Mkuu wa mkoa wa mbeya ameagiza halmashauri zote mkoa wa Mbeya kukamilisha utengenezaji wa madawati ifikapo JUNI 20 na sambamba na agizo hilo ametaadharisha juu ya takwimu za Madawati Hewa kwa lengo la kuficha ukweli 
Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo wilayani Mbarali wakati wa ziara ya kukagua utengenezaji wa madawati na hafla ya kukabidhi madawati 162 Shule ya msingi Jangurutu
Kwa takwimu zilizopo Mkoa wa Mbeya una upungufu wa madawati 32,000 na mpaka sasa utengenezaji wa madawati umefikia asilimia 95 na ametoa hadi tarehe 20 juni kila halmashauri iwe imekamilisha
Kuhusu udhibiti wa takwimu za madawati hewa ameagiza kila Mkuu wa shule apokee madawati kwa maandishi na yenye ubora kwa idadi Ile ile iliyobainishwa awali kuwa Ndiyo upungufu wa madawati katika Shule zao
Amewataka wanafunzi na walimu kuyatunza madawati wanayokabidhiwa ili kutoa nafasi kwa serikali, wadau na wananchi kushughulikia changamoto zingine kama ujenzi wa nyumba za walimu,madarasa na vyoo.     

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »