MALINZI AMPONGEZA MWENDA WA FKF

February 11, 2016

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Rais mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Kenya (FKF), Nick Mwendwa kwa kuchaguliwa kuliongoza shirikisho hilo.
Katika salamu hizo, Malinzi amempongeza Mwendwa kwa nafasi hiyo aliyopewa kuliongoza soka la nchini Kenya, na kuahidi TFF itaendelea kushirikiana nae katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Nick Mwendwa alishinda nafasi hiyo jana katika uchaguzi uliofanyika jijini Nairobi kwa kupata alama 50 kati ya 77 za wapiga kura wote na kupata nafasi hiyo iliyokua inashikiliwa na Samwel Nyamweya aliyemaliza muda wake.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »