WANANCHI CHANGAMKIENI SMART 6 MPYA YA VODACOM

October 22, 2015

 Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(kushoto)akiwanesha  waandishi wa habari(hawapo pichani) simu mpya aina ya Smart 6 wakati wa uzinduzi wa simu hiyo yenye kioo kikubwa kinachomuwezesha mtumiaji kusoma na kuangalia taarifa kwa urahisi na ina kamera ya kisasa na uwezo zaidi wa kuperuzi intanet ya 3G,itapatikana kwa bei nafuu kabisa shilingi
90,000/- inapatikana katika maduka yote ya kampuni hiyo.Mteja yeyote atakayenunua simu hiyo atajipatia ofa kabambe kabisa ya kupata 500MB bure na uwezo wa kutuma jumbe fupi za maneno zipatazo 200 kila mwezi kwa kipindi cha miezi 6 bure.Kulia ni Mkuu wa huduma na bidhaa wa kampuni hiyo,Samson Mwongela. 
KATIKA kuhakikisha wateja wake kutokuwa nyuma kiteknolojia na kupata huduma bora za mawasiliano ya kisasa kwa kutumia mtandao wa intanet,kampuni ya Vodacom Tanzania imezindua simu mpya ya Smart 6 ya gharama nafuu ambayo wananchi wengi wanaweza kumudu kuinunua.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa simu hii Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo,Kelvin Twissa amesema kuwa simu hii  imelenga wateja wake wenye vipato vya kawaida ili kuwawezesha kufurahia huduma za kisasa za matumizi ya simu za mkononi za Smartphone ili waweze kwenenda na teknolojia.

“Vodacom siku zote tumekuwa tukiwasikiliza wateja wetu na ndio maana tumeingiza sokoni simu hii ili kuwawezesha kufurahia matumizi ya simu za kisasa za smart ambazo zinawawezesha kupata huduma za internet na program nyinginezo za kurahisisha maisha yao na kuwa murua ikiwemo kupiga picha wazipendazo kwa kutumia simu zao,”Alisema Twissa.

Aliongeza kuwa simu hii ya Smart 6 ambayo itakuwa inauzwa kwa bei nafuu kabisa ya shilingi 90,000/- ina kioo kikubwa kinachomuwezesha mtumiaji kusoma na kuangalia taarifa kwa urahisi,ina kamera ya kisasa,uwezo zaidi wa kuperuzi intanet ya 3G, nafasi kubwa ya kuweka kumbukumbu na inakaa na betri kwa muda mrefu. Hii ni simu ya kipekee ambayo kila mteja anatakiwa kuwa nayo.

Alisema simu hizi zinapatikana katika maduka yote ya Vodacom na katika matamasha yote yanayofanywa na kampuni yetu nchi nzima ya Vodacom tumekufikia.Mteja yeyote atakayenunua simu hii atajipatia ofa kabambe kabisa ya kupata 500MB bure na uwezo wa kutuma jumbe fupi za maneno zipatazo 200 kila mwezi kwa kipindi cha miezi 6 bure.

Aliwataka wateja wa Vodacom na wananchi wengine kwa ujumla kuchangamkia fursa hii na kukamata Smart 6 kwa gharama nafuu ili kuendelea kupata taarifa za huduma mbalimbali zinazopatikana kwa kuperuzi mtandao wa intanet.Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti yetu www.vodacom.co.tz au kurasa zetu za Facebook na Twitter.
 Mkuu wa huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania,Samson Mwongela(kulia)akimshuhudia Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(kushoto)akiwanesha  waandishi wa habari(hawapo pichani) simu mpya aina ya Smart 6 wakati wa uzinduzi wa simu hiyo yenye kioo kikubwa kinachomuwezesha mtumiaji kusoma na kuangalia taarifa kwa urahisi na yenye kamera ya kisasa na uwezo zaidi wa kuperuzi intanet ya 3G, itapatikana kwa bei nafuu kabisa shilingi 90,000/- inapatikana katika maduka yote ya kampuni hiyo.Mteja yeyote atakayenunua simu hiyo atajipatia ofa kabambe kabisa ya kupata 500MB bure na uwezo wa kutuma jumbe fupi za maneno zipatazo 200 kila mwezi kwa kipindi cha miezi 6 bure.
 Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(kushoto) pamoja na Mkuu wa huduma na bidhaa wa Vodacom Tanzania,Samson Mwongela,wakijipiga selfiii kwa kutumia simu mpya aina ya Smart 6 waliyoizindua leo yenye kioo kikubwa kinachomuwezesha mtumiaji kusoma na kuangalia taarifa kwa urahisi na yenye kamera ya kisasa na uwezo zaidi wa kuperuzi intanet ya 3G, itapatikana kwa bei nafuu kabisa shilingi 90,000/- katika maduka yote ya kampuni hiyo.Mteja yeyote atakayenunua simu hiyo atajipatia ofa kabambe kabisa ya kupata 500MB bure na uwezo wa kutuma jumbe fupi za maneno zipatazo 200 kila mwezi kwa kipindi cha miezi 6 bure.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »