Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi
ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananch baada ya kuwasili
kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Oktoba 12, 2015, kwenye Viwanja
vya Nyawilimilwa, jimbo la Geita Vijijini mkoani Geita. Kushoto ni
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita ambaye pia ni Mgombea Ubunge wa jimbo
hilo, Joseph Kasheku maarufu kwa jina la King Msukuma.
Mgombea Ubunge jimbo la Geita
Vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Joseph Kasheku
‘King Msukuma’ akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni
uliofanyika katika Viwanja vya Nyawilimilwa, jimbo la Geita Vijijini
mkoani Geita, Oktoba 12, 2015.
William Mabula aliyekuwa Mgombea
Ubunge jimbo la geita mjini kwa tiketi ya Chadema, lakini chama hichi
kikamuengua dakika za mwisho baada ya kushinda kura za maoni kisha
kupachikwa mwingine aliyehamia chama hicho kutoka CCM, akitangaza
kuhamia CCM wakati wa mkutano wa kampeni uliofanywa na Mgombea Mwenza wa
Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika jimbo hiko
mkoani Geita, jana, Oktoba 12, 2015.
Mgombea Ubunge jimbo la Geita
mjini, Costantine Kanyasu, akiomba kura wakati wa mkutano wa kampeni
uliofanywa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, katika jimbo
hilo mkoani Geita, jana, Oktoba 12, 2015.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa
tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassa, akimuonyesha tukio la
kufurahisha, Mjumbe wa Kamati ya kampeni za CCM, Christopher Ole
Sendeka, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Oktona 12, 2015,
kwenye Viwanja vya Nyawilimilwa, jimbo la Geita Vijijini mkoani Geita.
Wananchi wakimshangilia Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan, katika
mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Geita mjini mkoani,
Geita.
Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva
anayeko katika kundi la Nimestuka, Juma Kiroboro maarufu kwa jina la
Juma Nature, akishambulia jukwaa akiwa na Ispekta Haruna wakati wa
mkutano wa kampeni wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,
uliofanyika jana, Oktoba 12, 2015, katika jimbo la Geita mjini mkoani
Geita.
Msanii Ashura Mohammed, aliyeko
katika kundi la Nimestuka, akionyesha umahiri wake wa kucheza muziki,
wakati kundi hilo lilipoburudisha wananchi katika mkutano wa kampeni
uliofanyika jana, Oktoba 12, 2015
Picha na Bashir Nkoromo