![]() |
Waumini wa dini ya Kislaamu Mkoani Tanga wakiwa kwenye ghafla ya kuchinja ng’ombe hamsini waliotolewa na wahisani REFSO kutoka nchini Uturuki kwa ajili ya siku kuu hiyo |
Waislamu nchini wametakiwa kuwa na
utamaduni wa kuwasaidia waumini wasio jiweza katika kutekeleza ibada tukufu ya
Eid –el Haj,inayoambatana na kuchinja ili wote wawe miongoni mwa
waliopata razi za Mwenyezi Mungu.
Wito huo ulitolewa jana kwenye ghafla
ya kuchinja ng’ombe hamsini waliotolewa na wahisani REFSO kutoka
nchini Uturuki kwa ajili ya siku kuu hiyo na Mwenyekiti wa Umoja wa Wasomi
wa Kiislamu Mkoa Tanga(Tampro), Nyumbwe Mwariko ambapo alisema jambo hilo ni
kheri kwa umma wa kiislam na wameipokea kama changamoto.
Mwariko akiwa katika shughuli hiyo
katika viwanja Neema Jijini Tanga alisema kuwa tangu mwaka 2010 wahisan
hao kutoka Uturuki wamekuwa mstari wa mbele kuwajali waislam wasiojiweza hapa
nchini na kushirikiana nao katika ibada hiyo na kutoa idadi kubwa ya ng’ombe
kwa mikoa kumi nchi nzima .
Aidha alisema ndani ya nchi yetu
hususan mkoa wwetu wa Tanga wapo watu waliokuwa na uwezo mkubwa lakini kwa
kutokuthamini umoja,mapenzi ,mshikamano kwa umma wa kiislam kumepelekea kujenga
matabaka.
“Niseme hakuna waislam Mwenyezi Mungu aliowaruzuku,
ni kutokuwa na imani ndani ya mioyo yao na kusababisha kutowajali wale
wasiojaaliwa” alisema Mwariko.
Hata hivyo alisema chama hicho
kwa kushirikiana na REFSO ya nchini Uturuki wamejipanga kutekeleza ibada hiyo
kila mwaka kwa ufanisi zaidi ili kuwasaidia waislam wote wasiojiweza mkoa mzima
wa Tanga kwa siku hiyo adhwimu ya Eid El haji.
EmoticonEmoticon