MTANDAO WA EVERJOBS TANZANIA KUWAKUTANISHA WAAJIRIWA NA WAAJIRI

September 16, 2015

 Mkurugenzi Mtendaji wa Everjobs wa Ukanda wa Afrika Eric Lauer, akiwaelezea waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa jinsi mfumo wao wa tovuti ambao unaweza kuwaunganisha waajiri na waajiriwa kwa urahisi kabisa huku waajiri wakipata nafasi ya kuweza kupata taarifa zote muhimu kutoka kwa wanaoomba kazi kupitia tovuti hiyo pindi wanapokuwa wamejiunga na Kampuni ya Everjobs Tanzania.Mkutano huo ulifanyika jana katika hoteli ya Serena Jijini Dar Es salaam.
 Mkurugenzi wa Everjobs Tanzania, Florens Roell akielezea namna ambavyo waajiri na waajiriwa wanaweza kunufaika na Kampuni ya Everjobs Tanzania ambayo inatoa nafasi kwa waajiriwa kuweza kuomba kazi kupitia tovuti yao ya www.everjobs.co.tz.
 Mkuu wa Kitengo cha Mauzo wa Everjobs Tanzania Lucas Masson (wa pili kutoka kulia) akielezea jinsi ya waajiliwa ambavyo wanaweza kujiunga katika tovuti yao ya www.everjobs.co.tz na kuweza kuona nafasi za kazi mbalimbali zinazotangazwa kupitia tovuti hiyo na kuweza kuomba kazi hapo hapo kupitia tovuti.
Mmoja wa wageni waalikwa akiuliza swali kwa Wakurugenzi na maafisa wa Everjobs wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa uliofanyika jana
  Mkurugenzi Mtendaji wa Everjobs Katika Ukanda wa Afrika Eric Lauer (wa kwanza kushoto) akijibu baadhi ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria mkutano uliofanyika jana katika hoteli ya Serena Jijini Dar
 Mmoja wa wageni akitoa shukrani kwa wamuluki wa kampuni ya Everjobs Tanzania kwa kuona changamoto na kuifanya kuwa fursa.
  
Baadhi ya Wageni waalikwa na waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mkutano huo

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »