MGOMBEA ubunge CCM -Namelock Sokoine AHIDI KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI MONDULI

September 29, 2015

Na Mahmoud Ahmad,Monduli
Mgombea ubunge wa jimbo  Monduli Bi,Namelock Sokoine kwa tiketi ya Chama cha mapinduzi (ccm)  amewaahidi wananchi pindi watakapo mpa ridhaa ya kuwa mgunge wao atahakikisha anamaliza kabisa migogoro ya ardhi katika jimbo hilo ambayo imekuwa kero ya muda mrefu na hata kupelekea  hata mifugo kuwa kutokana na hali hiyo na kupunguza jitihada za za waanchi kujiletea maendeleo yao kupitia kilimona ufugaji.
Hayo ameyasema jana katika uzinduzi wa kampeni ya ubunge katika jimbo la Monduli  iliyofanyika katika viwanbja vya soko la Nanja katika kata ya Nanja iliyoko wilaya ya Monduli ,mkoani Arushana kuhudhuriwa na maelfuya watu katika viwanja hivyo.
Hata hivyo aliongeza kuwa endapo wananchi watamchagua atataua matatizo yao yote kwa ikiwemo viwanja vyote vya monduli vitapimwa ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima ambayo imekuwa ikiwagharimu wananchi wake na kusababisha matatizo mbalimbali ameahidi kuyatatu kwa kipindi kifupi mara baada ya kuapiushwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Bi,Namelock alisema  jimbo la monduli limekuwa na tatizo loa uhaba wa maji ambayo ameahidi kulitatua kwa kiindi kifupi na suala la maji kulipa kipaumbele ili kuweza kuondoa kero ya maji katika jimbo hilo ili kuweza kuongeza shughuli za uzalishaji mali ili kuweza kuwaongezea kipato wananchi wake na kupambana na adui umaskini uliopo.
Mbali na hayo mgombea huyo ameahidi neema kwa wakazi na monduli na viunga vyake na ataweza kujenga kiwanda cha ngozi ili kuweza kuwanufaisha wafugaji pindi wanapovuna mifugoyao kwa matumizi mbalimbali kuweza kutumia kiwanda hicho kwa kuongeza ngozi thamani ili kuweza kupata bei kubwa ya ngozi kwa viwanda vya ndani na nje ya nchi kwa lengo la kukuza kipato cha mfugaji na kujiongezea kipato kuanzia ngazi ya familia hadi taifa.
Mbunge Namelock ameahidi kutoa kipaumbele kwa vijana  kupewa viwanja katika jimbo hilo ili kuweza kuwawezesha kujiendeleza na kupata  makazi bora na yakisasa ili kuwarahisishia ugumu wa maisha ya sasa na badae kwa vcizazi vyao sambamba na kuboresha sekta ya afya na elimu ili kumkwamua katika maisha ya sasa.
Awali akizindua kampeni hiyo ya mbunge huyo,Waziri wa Katiba na sheria Bi,Asharose Migiro  aliwataka wapiga kura kuweza kuchagua wagombea wa chama cha mapinduzi iliuweza kuletewa maendeleo yao kuanzia ngazi ya kata hadi jimbo ili kuweza kutataua changamoto mbalimbali katiuka eneo hilo ikiwemo uhaba wa chakula,mikopo kwa akina mama na vijana hususani a boda boda ili kuweza kuwapatia mikopo ya haraka ili kuwezaq kujiletea maendeleo yao kwa kuzalisha mali na kufanya biashara mbalimbali na kuweza kujiajiri kupambana na ukosefu wa ajira ulioko sasa.
Ambapo alisema kuwa wagombea wa ccm anatekeleza iolani ya chama chao kwa kuwaletea maendeleo ya haraka kulingana na mahitaji yao na changamoto zilizoko katika maeneo yao na hata kuendeleza ilani hiyopale ilipofikia kwa kuwaletea maendeleo yao.
Ambapo alitolea mfano ndchi nyingi za Afrika hajizamaliza kutatua matatizo katika jamiii zao lakini kinachofanyika nimuendleo na mikakakati thabiti ya ushirikiano wa kutatua matatizo ya wananchi wao  na mbali ya hivyo azma ya Serikali ya Tanzania nikurejesha mashamba yote kwa wananchi hasa maeneo ya wafugaji ili kuweza kulisha mifugo yao na kuongeza jitihada za dhati katika kuzalisha mifugo yao na kuondoa migogoro isiyo ya lazima baina ya wafugaji na wakulima iliyoko sasa.
Pia amewataka wananchi kuweza kchagua Namelock siku ya uchaguzi kwani yy ndie mbunge pekee ambae anaweza kutekeleza ahadi zake kwa makini kwa kushirikaina na Serikali na viongozi wake na kuweza kutafuta vyanzo mbadala vya umeme ili kuweza kuwaletea wananchi maedneleo na kuweza kuendnakarne ya sayansi na teknolojia iliyokosasa.
Kwa upande wake mmoja wa kada wa ccm Bi,Vaileth Mfuko  wakiwa wanamnadi mbunge huyo aliwataka wapiga kura kuweza kumchagua mbunge huyo kwani ni kiongozi bora ambae atawaletea mabadiliko na maendeleo ya kweli katika jimbo hilo kwani awali alishatoa vifaa vya kisasa vya hospitali katika jimbo hilo na kuboresha sekta ya Afya na wananchi hao kupata huduma kwa wakati na ambazo wanahitaji.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »