Kozi ya makocha wa CAF ya Leseni B iliyokua ifanyike kwa muda wa
wiki tatu mwezi Septemba mwaka huu kisiwani Zanzibar sasa imefutwa
kufuatia kupeleka mpira mahakamani.
Sasa kozi hiyo itafanyika tena pindi kesi ya mpira itakapoondelewa
mahakamani. Kumekua na hali ya kutokuelewana kwa uongozi wa Chama cha
Mpira wa Miguu kisiwani Zanzibar (ZFA) hali iliyopelekea uongozi wa ZFA
kupelekwa mahakamani.
Kwa mujibu wa kanuni za FIFA, masuala ya mpira wa miguu hayapaswi kupelekwa mahakamani